< Sefania 2 >

1 Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja, enyi taifa lisilo na aibu,
Tager eder sammen, og samler eder, du Folk, som ikke følte Skam!
2 kabla ya wakati ulioamriwa haujafika na siku ile inayopeperusha kama makapi, kabla hasira kali ya Bwana haijaja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana haijaja juu yenu.
førend Beslutningen vorder udført — som Avner farer Dagen frem — førend Herrens brændende Vrede kommer over eder, førend Herrens Vredes Dag kommer over eder!
3 Mtafuteni Bwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi, ninyi ambao hufanya lile analoamuru. Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu; labda mtahifadhiwa siku ya hasira ya Bwana.
Søger Herren, alle I sagtmodige i Landet, som holde hans Lov! søger Retfærdighed, søger Sagtmodighed, maaske kunne I blive skjulte paa Herrens Vredes Dag!
4 Gaza utaachwa na Ashkeloni utaachwa magofu. Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu na Ekroni utangʼolewa.
Thi Gaza skal blive forladt, og Askalon skal blive til Øde; Asdod skal man uddrive om Middagen, og Ekron skal oprykkes med Rod.
5 Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari, enyi Wakerethi; neno la Bwana liko dhidi yenu, ee Kanaani, nchi ya Wafilisti. “Mimi nitawaangamiza, na hakuna atakayebaki.”
Ve dem, som bebo Egnen ved Havet, Kreternes Folk! Herrens Ord er over eder, du Kanaan, Filisternes Land! og jeg vil ødelægge dig, at ingen skal bo der.
6 Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi, patakuwa mahali pa wachungaji na mazizi ya kondoo.
Og Egnen ved Havet skal være til Boliger, som Hyrder udgrave sig, og til Faarefolde.
7 Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda, hapo watapata malisho. Wakati wa jioni watajilaza chini katika nyumba za Ashkeloni. Bwana Mungu wao atawatunza, naye atawarudishia wafungwa wao.
Og det skal blive en Egn for de overblevne af Judas Hus, paa den skulle de græsse; i Askalons Huse skulle de hvile om Aftenen; thi Herren, deres Gud, skal besøge dem og omvende deres Fangenskab.
8 “Nimeyasikia matukano ya Moabu nazo dhihaka za Waamoni, ambao waliwatukana watu wangu na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.
Jeg har hørt Moabs Spot og Ammons Børns Forhaanelser, med hvilke de forhaanede mit Folk og ophøjede sig storlig imod dets Landemærke.
9 Hakika, kama niishivyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, “hakika Moabu itakuwa kama Sodoma, Waamoni kama Gomora: mahali pa magugu na mashimo ya chumvi, nchi ya ukiwa milele. Mabaki ya watu wangu watawateka nyara; mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”
Derfor, saa sandt jeg lever, siger den Herre Zebaoth, Israels Gud: Moab skal blive som Sodoma og Ammons Børn som Gomorra, et Hjem for Nælder og en Saltgrav og en Ørk til evig Tid; de overblevne af mit Folk skulle plyndre dem, og Levningen af mit Folk skal arve dem.
10 Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao, kwa kutukana na kudhihaki watu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Dette skal ske dem for deres Hovmods Skyld, fordi de haanede, saa at de ophøjede sig storlig over den Herre Zebaoths Folk.
11 Bwana atakuwa wa kuhofisha kwao atakapoangamiza miungu yote ya nchi. Mataifa katika kila pwani yatamwabudu, kila moja katika nchi yake.
Forfærdelig skal Herren være over dem, thi han skal lade alle Jordens Guder svinde hen; og de skulle tilbede ham, enhver fra sit Sted, alle Hedningernes Øer.
12 “Ninyi pia, ee Wakushi, mtauawa kwa upanga wangu.”
Ogsaa I, Morianer! skulle være iblandt dem, som ere ihjelslagne ved mit Sværd.
13 Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini na kuangamiza Waashuru, akiiacha Ninawi ukiwa na pakame kama jangwa.
Han skal og udrække sin Haand imod Norden og ødelægge Assyrien og gøre Ninive til et Øde, til et tørt Land som Ørkenen.
14 Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale, viumbe vya kila aina. Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba wataishi juu ya nguzo zake. Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani, kifusi kitakuwa milangoni, boriti za mierezi zitaachwa wazi.
Og Hjorde skulle ligge midt derudi, alle Slags vilde Dyr i Flok, baade Rørdrum og Pindsvin skulle tilbringe Natten paa dens Søjlehoveder; en Lyd af syngende høres i Vindueshullerne, Grus ligger over Dørtærskelen; thi dens Cederpanel har han blottet.
15 Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha wakijisikia salama. Ulisema moyoni mwako, “Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.” Jinsi gani umekuwa gofu, mahali pa kulala wanyama pori! Wote wanaopita kando yake wanauzomea na kutikisa mkono kwa dharau.
Dette er den jublende Stad, som boede tryggelig, som sagde i sit Hjerte: Jeg, og ingen uden jeg; hvorledes er den bleven til et Øde, et Leje for vilde Dyr? hver, som gaar forbi den, vil spotte og ryste sin Haand.

< Sefania 2 >