< Sefania 1 >

1 Neno la Bwana lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:
[I am] Zephaniah, the son of Cushi, the grandson of Gedaliah, and the great-grandson of Amariah, whose father was [King] Hezekiah. Yahweh gave this message to me during the time when [King] Amon’s son Josiah was the King of Judah.
2 Bwana asema, “Nitafagia kila kitu kutoka kwenye uso wa dunia.”
Yahweh says, “I will (sweep away/destroy) everything [HYP] that is on the earth.
3 “Nitafagilia mbali watu na wanyama; nitafagilia mbali ndege wa angani na samaki wa baharini. Wafanyao maovu watapata tu kokoto, nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,” asema Bwana.
I will sweep away people and animals. I will sweep away birds and fish. I will get rid of wicked people; there will be no more [wicked] [HYP] people on the earth.”
4 “Nitaiadhibu Yuda na wote wakaao Yerusalemu. Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali kila mabaki ya Baali, majina ya wapagani na makuhani waabuduo sanamu:
“[These are some of the things that I will do]: I will punish the people who live in Jerusalem and [other places in] Judah. I will destroy everything that has been used in the worship of Baal. I will cause [people] to no longer remember the names of the pagan priests or the [other] priests [who have turned away from me].
5 wale ambao husujudu juu ya mapaa kuabudu jeshi la vitu vya angani, wale ambao husujudu na kuapa kwa Bwana na ambao pia huapa kwa Malkamu,
[I will get rid of] those who go up on the roofs [of their houses] and worship the sun and moon and stars, those who claim that they worship me but [also] worship [their god] Molech.
6 wale wanaoacha kumfuata Bwana, wala hawamtafuti Bwana wala kutaka shauri lake.
I will get rid of all those who previously worshiped me but no longer do, those who no [longer] seek my [help or ask me to tell them what they should do.”]
7 Nyamazeni mbele za Bwana Mwenyezi, kwa maana siku ya Bwana iko karibu. Bwana ameandaa dhabihu, amewaweka wakfu wale aliowaalika.
Be silent in front of Yahweh the Lord, because it will soon be the time/day when Yahweh [will judge and punish people]. Yahweh has prepared to get rid of [the people of Judah]; they will be like [MET] animals that are slaughtered for sacrifices, and he has chosen [their enemies] to be the ones who will get rid of them.
8 Katika siku ya dhabihu ya Bwana nitawaadhibu wakuu na wana wa mfalme na wale wote wanaovaa nguo za kigeni.
Yahweh says, “On that day when I will get rid of [the people of Judah], [I will punish] their officials and the king’s sons, and [I will punish] all those who worship foreign gods [MTY].
9 Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao hukwepa kukanyaga kizingiti, ambao hujaza hekalu la miungu yao kwa dhuluma na udanganyifu.”
I will punish those who [show that they revere their god Dagan] by avoiding stepping on the threshold [of his temple], and those who do violent things and tell lies in the temples of their gods.”
10 Bwana asema, “Katika siku hiyo kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki, maombolezo kutoka mtaa wa pili, na mshindo mkubwa kutoka vilimani.
Yahweh [also] says, “On that day, people will cry [out] at the Fish Gate [of Jerusalem]. People will wail in the newer part of the city, and [people will hear] a loud crash [of buildings collapsing] in the hills.
11 Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni; wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa, wote ambao wanafanya biashara ya fedha wataangamizwa.
[So, all you] people who live in the market area [of Jerusalem] should wail, because all those who sell goods and weigh out silver will be slaughtered.
12 Wakati huo nitasaka mji wa Yerusalemu kwa taa, na kuwaadhibu wale ambao wanakaa katika hali ya kuridhika, ambao ni kama divai iliyobaki kwenye machicha, ambao hudhani, ‘Bwana hatafanya lolote, jema au baya.’
[It will be as though] I will light lanterns to search in [dark places in] Jerusalem for those who have become very satisfied with their behavior and complacent [about their sins]. They think that [I], Yahweh, will do nothing to them, neither good things nor bad things.
13 Utajiri wao utatekwa nyara, nyumba zao zitabomolewa. Watajenga nyumba, lakini hawataishi ndani yake; watapanda mizabibu lakini hawatakunywa divai yake.
[But I say that] their valuable possessions will be plundered/stolen [by their enemies], and their houses will be destroyed. They will build [new] homes, but they will not live in them; they will plant vineyards, but they will never drink [any] wine [made from grapes that grow there].”
14 “Siku kubwa ya Bwana iko karibu: iko karibu na inakuja haraka. Sikilizeni! Kilio katika siku ya Bwana kitakuwa kichungu, hata shujaa atapiga kelele.
It will soon be the day/time when Yahweh [will punish people]. It will be here quickly. It will be a time [when people cry] bitterly, a time when [even] brave soldiers will cry loudly.
15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, siku ya fadhaa na dhiki, siku ya uharibifu na ukiwa, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene,
It will be a time when [God shows that he is] very angry, a time when [people experience much] distress/suffering and trouble. [It will be] a time [when many things are] ruined and destroyed [DOU]. It will be a time when it is very gloomy and dark [DOU], when the clouds are very black.
16 siku ya tarumbeta na mlio wa vita dhidi ya miji yenye ngome na dhidi ya minara mirefu.
It will be a time when [soldiers] will blow trumpets [to call other soldiers] to battle. [Your enemies] will tear down the walls around your cities and the high towers [at the corners of those walls].
17 Nitawaletea watu dhiki, nao watatembea kama vipofu, kwa sababu wametenda dhambi dhidi ya Bwana. Damu yao itamwagwa kama vumbi na matumbo yao kama taka.
Because you sinned against Yahweh, he will cause you to experience great distress; you will walk [around groping] like [SIM] blind people do. Your blood will flow [from your bodies] like [SIM] water, and your corpses will lie on the ground and rot [SIM].
18 Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana. Katika moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, kwa maana ataleta mwisho wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”
At the time that [Yahweh shows that he] is very angry [with you], you will not be able to save yourselves by [giving] silver or gold [to your enemies]. Because Yahweh (is very jealous/does not want people to worship any other god), he will send a fire to burn up the entire world, and he will suddenly get rid of all the [wicked] people who live on the earth.

< Sefania 1 >