< Zekaria 1 >

1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
I den ottende Måned i Darius's andet Regeringsår kom HERRENs Ord til Profeten Zakarias, en Søn af Berekja, en Søn af Iddo, således:
2 “Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
HERREN var fuld af Harme imod eders Fædre.
3 Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Men sig til dem: Så siger Hærskarers HERRE: Vend om til mig, lyder det fra Hærskarers HERRE, så vil jeg vende om til eder, siger Hærskarers HERRE.
4 Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
Vær ikke som eders Fædre, til hvem de tidligere Profeter talte således: Så siger Hærskarers HERRE: Vend om fra eders onde Veje og onde Gerninger! Men de hørte ikke og ænsede mig ikke, lyder det fra HERREN.
5 Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
Eders Fædre, hvor er de? Og Profeterne, lever de evigt?
6 Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
Men mine Ord og Bud, som jeg overgav mine Tjenere Profeterne, nåede de ikke eders Fædre, så de måtte vende om og sige: "Som Hærskarers HERRE havde sat sig for at gøre imod os for vore Vejes og Gerningers Skyld, således gjorde han."
7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
På den fire og tyvende dag i den ellevte Måned, det er Sjebat Måned, i Darius's andet Regeringsår kom HERRENs Ord til Profeten Zakarias, en Søn af Berekja, en Søn af Iddo, således:
8 Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
Jeg skuede i Nat, og se, en Mand på en rød Hest holdt mellem Bjergene ved den dybe Kløft, og bag ham var der røde, mørke, hvide og brogede Heste.
9 Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
Jeg spurgte: "Hvad betyder de, Herre?" Og Engelen, som talte med mig, sagde: "Jeg vil vise dig, hvad de betyder."
10 Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
Så tog Manden, som holdt mellem Bjergene, til Orde og sagde: "Det er dem, HERREN udsender, for at de skal drage Jorden rundt."
11 Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
Og de tog til Orde og sagde til HERRENs Engel, som stod mellem Bjergene: "Vi drog Jorden rundt, og se, hele Jorden er rolig og stille.
12 Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
HERRENs Engel tog da til Orde og sagde: "Hærskarers HERRE! Hvor længe varer det, før du forbarmer dig over Jerusalem og Judas Byer, som du nu har været vred på i halvfjerdsindstyve År?"
13 Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
Og til Svar gav HERREN Engelen, som talte med mig, gode og trøstende Ord.
14 Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
Engelen, som talte med mig, sagde så til mig: Tal og sig: Så siger Hærskarers HERRE: Jeg er fuld af Nidkærhed for Jerusalem og Zion
15 lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
og af Harme mod de trygge Hedninger, fordi de hjalp til at gøre Ulykken stor, da min Vrede kun var lille.
16 “Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Derfor, så siger HERREN: Jeg vender mig til Jerusalem og forbarmer mig over det; mit Hus skal opbygges der, lyder det fra Hærskarers HERRE, og der skal udspændes Målesnor over Jerusalem.
17 “Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
Tal videre: Så siger Hærskarers HERRE: Mine Byer skal atter strømme med Velsignelse, og HERREN vil atter trøste Zion og udvælge Jerusalem.
18 Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
Derpå løftede jeg mine Øjne og skuede, og se, der var fire Horn.
19 Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
Jeg spurgte Engelen, som talte med mig: "Hvad betyder de?" Han svarede: "Det er de Horn, som har spredt Juda, Israel og Jerusalem."
20 Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
Så lod HERREN mig se fire Smede.
21 Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”
Jeg spurgte: "Hvad kommer de for?" Og han svarede: "Hine er de Horn, som spredte Juda, så det ikke kunde løfte sit Hoved; og nu kommer disse for at hvæsse Økser til at slå Hornene til Jorden på de Hedninger, som løftede deres Horn mod Judas Land for at sprede det."

< Zekaria 1 >