< Zekaria 1 >

1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
Darius kah a kum bae, a hla rhet vaengah, Iddo koca Berekiah capa tonghma Zekhariah taengah BOEIPA ol cet tih,
2 “Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
“BOEIPA he a thintoek tih na pa rhoek taengah thinhulnah om.
3 Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Te dongah amih te thui pah. Caempuei BOEIPA loh he ni a thui. He tah caempuei BOEIPA kah olphong ni. Caempuei BOEIPA loh, “Kai taengla ha mael uh lamtah nangmih taengla ka mael ni,” a ti.
4 Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
Na pa rhoek bangla om uh boeh. Amih te tonghma lamhma rhoek loh a khue uh tih, “Caempuei BOEIPA loh he ni a thui na longpuei thae lamloh mael uh laeh. Na khoboe neh na khoboe thae rhoe mah,’ a ti. Tedae hnatun uh pawt tih kai taengah a hnatung uh moenih. He tah BOEIPA kah olphong ni.
5 Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
Na pa rhoek te melae? Tonghma rhoek khaw kumhal ah hing uh nim?
6 Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
Ka ol neh ka oltlueh he ka sal tonghma rhoek ka uen dae ta. Na pa rhoek loh kae uh pawt tih nim a mael uh? Te vaengah, “Mamih kah longpuei bangla mamih taengah saii ham neh mamih kah khoboe bangla caempuei BOEIPA loh a mangtaeng tih mamih taengah a saii tangloeng coeng,’ a ti uh,” a ti nah.
7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
Darius kah a kum bae nah, hla hlai khat, Shebat hla hnin kul hnin li vaengah, BOEIPA ol te Iddo koca Berekiah capa tonghma Zekhariah taengla cet tih a thui.
8 Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
“Khoyin kah ka hmuh dongah hlang te marhang ling dongah tarha ana ngol. Anih te cuihal ding kah a cok ah pai. A hnukkah marhang rhoek tah a ling, a pol neh a bok om.
9 Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
Te vaengah, “Ka boeipa balae he,” ka ti nah. Te vaengah kai taengah aka cal puencawn loh kai taengah, “Amih rhoek balae ti khaw kamah loh nang kan tueng eh?,” a ti.
10 Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
Te phoeiah cuihal ding kah aka pai hlang loh a doo tih, “He rhoek he diklai ah pongpa hamla BOEIPA loh a tueih coeng,” a ti.
11 Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
Te vaengah cuihal ding kah aka pai BOEIPA puencawn te a doo uh tih, “Diklai ah ka pongpa uh coeng dae diklai pum kah khosa khaw mong ngawn ke,” a ti uh.
12 Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
Te dongah BOEIPA kah puencawn loh a doo tih, “Caempuei BOEIPA aw, Jerusalem neh Judah khopuei rhoek te me hil nim na haidam pawt ve? Te te kum sawmrhih kosi na hong thil coeng,” a ti nah.
13 Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
Te dongah BOEIPA loh kai taengah aka cal puencawn te hloephoelhnah ol then ol neh a doo.
14 Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
Te phoeiah kai taengah aka cal puencawn loh kai taengah, “Khue lamtah, 'Caempuei BOEIPA loh he ni a thui. Jerusalem ham ka thatlai tih Zion ham khaw thatlainah len.
15 lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
Tedae kai he namtom hlang aka lawn taengah thinhul bat la ka thintoek. Ka thintoek khaw yol dae amih loh boethae te a koei uh.
16 “Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Te dongah BOEIPA loh he ni a thui. Jerusalem la haidamnah neh ka mael ni. A khuiah ka im a sak ni. He tah caempuei BOEIPA kah olphong ni. Jerusalem te rhilam rhui ka toe ni, 'ti nah.
17 “Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
Koep pang lamtah, 'Caempuei BOEIPA loh he ni a thui. Ka khopuei rhoek ah hnothen neh baesawt pueng ni. BOEIPA loh Zion te koep a hloep vetih Jerusalem te koep a coelh ni, ' a ti nah,” a ti.
18 Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
Te phoeiah ka mik te ka huel tih ka sawt hatah ki pali lawt ka hmuh.
19 Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
Te dongah kai taengah aka cal puencawn te, “Balae he?” ka ti nah. Tedae kai taengah, “He ki rhoek loh Judah, Israel neh Jerusalem a thaek,” a ti.
20 Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
Te phoeiah BOEIPA loh kai te kutthai pali n'tueng.
21 Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”
Te vaengah, “Amih aka lo long he balae a saii eh?” ka ti nah. Te dongah, “He rhoek kah ki loh Judah te a thaek uh tih hlang ol bangla a lu khaw dangrhoek thai pawh. Tedae Judah khohmuen aka tlai thil tih aka thaek ki, namtom kah ki te omtoem ham neh amih te lakueng sak hamla ha pai uh,” a ti.

< Zekaria 1 >