< Zekaria 7 >

1 Katika mwaka wa nne wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria siku ya nne ya mwezi wa tisa, mwezi wa Kisleu.
Et il arriva dans la quatrième année du roi Darius, que la parole du Seigneur fut adressée à Zacharie, au quatrième jour du neuvième mois, qui est appelé Casleu.
2 Watu wa Betheli walikuwa wamemtuma Shareza na Regem-Meleki pamoja na watu wao, kumsihi Bwana
Or Sarasar et Rogommélech et les hommes qui étaient avec lui, envoyèrent à la maison de Dieu pour implorer la face du Seigneur,
3 kwa kuwauliza makuhani wa nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na manabii, “Je, imempasa kuomboleza na kufunga katika mwezi wa tano, kama ambavyo nimekuwa nikifanya kwa miaka mingi?”
Afin de parler aux prêtres de la maison du Seigneur des armées et aux prophètes, en leur disant: Faut-il que je pleure dans le cinquième mois, ou dois-je me sanctifier comme je l’ai déjà fait pendant beaucoup d’années?
4 Kisha neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote likanijia kusema:
Et la parole du Seigneur des armées me fut adressée, disant:
5 “Waulize watu wote wa nchi na makuhani, ‘Je, mlipofunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba kwa miaka sabini iliyopita, mlifunga kweli kwa ajili yangu?
Parle à tout le peuple de la terre et aux prêtres, en disant: Lorsque vous avez jeûné et pleuré dans le cinquième et le septième mois, pendant ces soixante-dix années, est-ce pour moi que vous avez jeûné?
6 Na mlipokuwa mkila na kunywa, je, hamkuwa mnasherehekea kwa ajili ya nafsi zenu?
Et lorsque vous avez mangé et que vous avez bu, n’est-ce pas pour vous que vous avez mangé et pour vous que vous avez bu?
7 Je, haya sio maneno ya Bwana aliyosema kupitia manabii waliotangulia, wakati Yerusalemu pamoja na miji inayoizunguka ilipokuwa katika hali ya utulivu na ya mafanikio, wakati Negebu na Shefala zikiwa zimekaliwa na watu?’”
Ne sont-ce pas là les paroles qu’a dites le Seigneur par l’entremise des prophètes antérieurs, lorsque Jérusalem était encore habitée, et qu’elle était opulente, elle-même et les villes autour d’elle, et qu’au midi et dans la plaine tout était habité?
8 Neno la Bwana likamjia tena Zekaria:
Et la parole du Seigneur des armées fut adressée à Zacharie, disant:
9 “Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Fanyeni hukumu za haki, onyesheni rehema na huruma ninyi kwa ninyi.
Voici ce que dit le Seigneur des armées: Jugez selon la vérité, usez de miséricorde et de clémence, chacun envers son frère.
10 Msimwonee mjane wala yatima, mgeni wala maskini. Msiwaziane mabaya mioyoni mwenu ninyi kwa ninyi.’
Et n’opprimez point la veuve, ni l’orphelin, ni l’étranger, ni le pauvre; et qu’un homme ne médite pas dans son cœur le mal contre son frère.
11 “Lakini wakakataa kusikiliza, wakanipa kisogo kwa ukaidi na kuziba masikio yao.
Mais vos pères n’ont pas voulu être attentifs à ma voix, et ils ont détourné l’épaule en se retirant, et ils ont appesanti leurs oreilles pour ne pas entendre.
12 Wakaifanya mioyo yao migumu kama jiwe gumu na hawakuisikiliza sheria au maneno ambayo Bwana Mwenye Nguvu Zote aliyatuma kwa njia ya Roho wake kupitia manabii waliotangulia. Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote alikasirika sana.
Et leur cœur, ils l’ont rendu dur comme un diamant, pour ne pas écouter la loi et la parole que le Seigneur des armées leur envoya avec son esprit, par l’entremise de ses prophètes antérieurs; et le Seigneur des armées conçut une grande indignation.
13 “‘Wakati nilipoita, hawakusikiliza, kwa hiyo walipoita, sikusikiliza,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Or il est arrivé comme il a parlé, et ils n’ont pas écouté; ainsi ils crieront, et je ne les écouterai pas, dit le Seigneur des armées.
14 ‘Niliwatawanya kwa upepo wa kisulisuli miongoni mwa mataifa yote, mahali ambapo walikuwa wageni. Nchi ikaachwa ukiwa nyuma yao kiasi kwamba hakuna aliyeweza kuingia au kutoka. Hivi ndivyo walivyoifanya ile nchi iliyokuwa imependeza kuwa ukiwa.’”
Et je les ai dispersés dans tous les royaumes qu’ils ne connaissent pas; et leur terre a été désolée derrière eux, en sorte qu’il n’y avait personne qui y passât, et qui en revînt; et ils ont fait d’une terre délicieuse un désert.

< Zekaria 7 >