< Zekaria 7 >

1 Katika mwaka wa nne wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria siku ya nne ya mwezi wa tisa, mwezi wa Kisleu.
La quatrième année du roi Darius, la parole de Yahweh fut adressée à Zacharie, au quatrième jour du neuvième mois, en Casleu.
2 Watu wa Betheli walikuwa wamemtuma Shareza na Regem-Meleki pamoja na watu wao, kumsihi Bwana
Béthel avait envoyé Sarasar et Rogommélech, avec ses gens, pour implorer Yahweh,
3 kwa kuwauliza makuhani wa nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na manabii, “Je, imempasa kuomboleza na kufunga katika mwezi wa tano, kama ambavyo nimekuwa nikifanya kwa miaka mingi?”
pour parler aux prêtres de la maison de Yahweh des armées et aux prophètes, en ces termes: " Dois-je pleurer au cinquième mois, et faire abstinence, comme j'ai fait depuis tant d'années? "
4 Kisha neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote likanijia kusema:
La parole de Yahweh des armées me fut adressée en ces termes:
5 “Waulize watu wote wa nchi na makuhani, ‘Je, mlipofunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba kwa miaka sabini iliyopita, mlifunga kweli kwa ajili yangu?
Parle à tout le peuple du pays et aux prêtres, en ces termes: Quand vous avez jeûné et célébré le deuil au cinquième et au septième mois, et cela depuis soixante-dix ans, est-ce pour moi que vous jeûniez?
6 Na mlipokuwa mkila na kunywa, je, hamkuwa mnasherehekea kwa ajili ya nafsi zenu?
Et quand vous mangez et buvez, n'est-ce pas vous qui mangez et vous qui buvez?
7 Je, haya sio maneno ya Bwana aliyosema kupitia manabii waliotangulia, wakati Yerusalemu pamoja na miji inayoizunguka ilipokuwa katika hali ya utulivu na ya mafanikio, wakati Negebu na Shefala zikiwa zimekaliwa na watu?’”
N'y a-t-il pas les paroles qu'a proclamées Yahweh par l'intermédiaire des anciens prophètes, quand Jérusalem était habitée et tranquille, avec ses villes autour d'elle, et que le négéb et la sephélah étaient habités?
8 Neno la Bwana likamjia tena Zekaria:
La parole de Yahweh fut adressée à Zacharie en ces termes:
9 “Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Fanyeni hukumu za haki, onyesheni rehema na huruma ninyi kwa ninyi.
Ainsi parlait Yahweh des armées en disant: " Rendez la justice selon la vérité; pratiquez la miséricorde et la compassion chacun envers son frère;
10 Msimwonee mjane wala yatima, mgeni wala maskini. Msiwaziane mabaya mioyoni mwenu ninyi kwa ninyi.’
n'opprimez pas la veuve et l'orphelin, l'étranger et le pauvre, et me méditez pas l'un contre l'autre le mal dans vos cœurs. "
11 “Lakini wakakataa kusikiliza, wakanipa kisogo kwa ukaidi na kuziba masikio yao.
Mais ils ont refusé d'écouter, ils ont prêté une épaule rebelle et endurci leurs oreilles pour ne pas entendre.
12 Wakaifanya mioyo yao migumu kama jiwe gumu na hawakuisikiliza sheria au maneno ambayo Bwana Mwenye Nguvu Zote aliyatuma kwa njia ya Roho wake kupitia manabii waliotangulia. Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote alikasirika sana.
Ils ont rendu leur cœur tel que le diamant, pour ne pas entendre la loi et les paroles que Yahweh des armées leur adressait par son Esprit, par l'intermédiaire des anciens prophètes. Aussi y eut-il une violente indignation de la part de Yahweh des armées.
13 “‘Wakati nilipoita, hawakusikiliza, kwa hiyo walipoita, sikusikiliza,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Et il arriva: De même qu'il avait appelé sans qu'ils écoutassent, " de même ils appelleront sans que je les écoute, dit Yahweh des armées.
14 ‘Niliwatawanya kwa upepo wa kisulisuli miongoni mwa mataifa yote, mahali ambapo walikuwa wageni. Nchi ikaachwa ukiwa nyuma yao kiasi kwamba hakuna aliyeweza kuingia au kutoka. Hivi ndivyo walivyoifanya ile nchi iliyokuwa imependeza kuwa ukiwa.’”
Je les disperserai parmi toutes les nations qu'ils ne connaissent pas, et derrière eux le pays restera désolé, sans personne qui passe ou revienne. " D'un pays de délices ils ont fait un désert.

< Zekaria 7 >