< Zekaria 7 >

1 Katika mwaka wa nne wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria siku ya nne ya mwezi wa tisa, mwezi wa Kisleu.
And it is maad in the fourthe yeer of Darius, kyng, the word of the Lord was maad to Sacarie, in the fourthe dai of the nynthe monethe, that is Caslew.
2 Watu wa Betheli walikuwa wamemtuma Shareza na Regem-Meleki pamoja na watu wao, kumsihi Bwana
And Sarasar, and Rogumelech, and men that weren with hem, senten to the hous of the Lord, for to preye the face of the Lord;
3 kwa kuwauliza makuhani wa nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na manabii, “Je, imempasa kuomboleza na kufunga katika mwezi wa tano, kama ambavyo nimekuwa nikifanya kwa miaka mingi?”
that thei schulden seie to prestis of the hous of the Lord of oostis, and to profetis, and speke, Whether it is to wepe to me in the fyuethe monethe, ether Y schal halowe me, as Y dide now many yeeris?
4 Kisha neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote likanijia kusema:
And the word of the Lord was maad to me,
5 “Waulize watu wote wa nchi na makuhani, ‘Je, mlipofunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba kwa miaka sabini iliyopita, mlifunga kweli kwa ajili yangu?
and seide, Speke thou to al the puple of the lond, and to prestis, and seie thou, Whanne ye fastiden, and weiliden in the fyueth and seuenthe monethe, bi these seuenti yeeris, whether ye fastiden a fast to me?
6 Na mlipokuwa mkila na kunywa, je, hamkuwa mnasherehekea kwa ajili ya nafsi zenu?
And whanne ye eeten, and drunken, whether ye eten not to you, and drunken not to you silf?
7 Je, haya sio maneno ya Bwana aliyosema kupitia manabii waliotangulia, wakati Yerusalemu pamoja na miji inayoizunguka ilipokuwa katika hali ya utulivu na ya mafanikio, wakati Negebu na Shefala zikiwa zimekaliwa na watu?’”
Whether wordis of profetis ben not, whiche the Lord spak in the hond of the formere profetis, whanne yit Jerusalem was enhabited, and was ful of richessis, and it, and citees therof in cumpas therof, and at the south and in feeldi place was enhabited?
8 Neno la Bwana likamjia tena Zekaria:
And the word of the Lord was maad to Sacarie, and seide, The Lord of oostis saith these thingis, and spekith,
9 “Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Fanyeni hukumu za haki, onyesheni rehema na huruma ninyi kwa ninyi.
Deme ye trewe dom, and do ye merci, and doyngis of merci, ech man with his brother.
10 Msimwonee mjane wala yatima, mgeni wala maskini. Msiwaziane mabaya mioyoni mwenu ninyi kwa ninyi.’
And nyle ye falsli calenge a widewe, and fadirles, ether modirles, and comelyng, and pore man; and a man thenke not in his herte yuel to his brother.
11 “Lakini wakakataa kusikiliza, wakanipa kisogo kwa ukaidi na kuziba masikio yao.
And thei wolden not `take heede, and thei turneden awei the schuldre, and yeden awei, and `maden heuy her eeris, lest thei herden.
12 Wakaifanya mioyo yao migumu kama jiwe gumu na hawakuisikiliza sheria au maneno ambayo Bwana Mwenye Nguvu Zote aliyatuma kwa njia ya Roho wake kupitia manabii waliotangulia. Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote alikasirika sana.
And thei puttiden her herte as adamaunt, lest thei herden the lawe, and wordis whiche the Lord of oostis sente in his Spirit, bi the hond of the formere profetis; and greet indignacioun was maad of the Lord of oostis.
13 “‘Wakati nilipoita, hawakusikiliza, kwa hiyo walipoita, sikusikiliza,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And it is doon, as he spak; and as thei herden not, so thei schulen crie, and Y schal not here, seith the Lord of oostis.
14 ‘Niliwatawanya kwa upepo wa kisulisuli miongoni mwa mataifa yote, mahali ambapo walikuwa wageni. Nchi ikaachwa ukiwa nyuma yao kiasi kwamba hakuna aliyeweza kuingia au kutoka. Hivi ndivyo walivyoifanya ile nchi iliyokuwa imependeza kuwa ukiwa.’”
And Y scateride hem bi alle rewmes, whiche thei knewen not, and the lond is desolat fro hem; for that there was not a man goynge and turnynge ayen, and thei han put desirable lond in to desert.

< Zekaria 7 >