< Zekaria 5 >

1 Nikatazama tena: na hapo mbele yangu kulikuwa na kitabu kilichoruka!
And Y was conuertid, and reiside myn iyen, and siy, and lo! a book fleynge.
2 Akaniuliza, “Unaona nini?” Nikamjibu, “Naona kitabu kinachoruka chenye, urefu wa dhiraa ishirini na upana wa dhiraa kumi.”
And he seide to me, What seest thou? And Y seide, Lo! Y se a book fleynge; the lengthe therof was of twenti cubitis, and the breede therof of ten cubitis.
3 Akaniambia, “Hii ni laana inayotoka kwenda juu ya nchi yote, kwa kuwa kufuatana na yale yaliyoandikwa katika upande mmoja, kila mwizi atafukuziwa mbali, pia kufuatana na yaliyo upande wa pili, kila aapaye kwa uongo atafukuziwa mbali.
And he seide to me, This is the curs, that goith on the face of al erthe; for ech theef schal be demed, as it is writun there; and ech man swerynge, schal be demyd of this also.
4 Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, ‘Nitaituma hiyo laana, nayo itaingia katika nyumba ya mwizi na nyumba ya huyo aapaye kwa uongo kwa Jina langu. Itabaki katika nyumba yake na kuiharibu, pamoja na mbao zake na mawe yake.’”
Y schal lede out it, seith the Lord of oostis, and it schal come to the hous of a theef, and to the hous of hym that swerith falsli in my name; and it schal dwelle in myddil of hys hous, and schal waaste hym, and hise trees, and hise stoonys.
5 Kisha yule malaika aliyekuwa akizungumza nami akanijia na kuniambia, “Tazama juu uone ni nini kile kinachojitokeza.”
And the aungel wente out, that spak in me, and seide to me, Reyse thin iyen, and se, what this thing is, that goith out.
6 Nikamuuliza, “Ni kitu gani?” Akanijibu, “Ni kikapu cha kupimia.” Kisha akaongeza kusema, “Huu ni uovu wa watu katika nchi nzima.”
And Y seide, What is it? And he seide, This is a pot goyng out. And he seide, This is the iye of hem in al erthe.
7 Kisha kifuniko kilichotengenezwa kwa madini ya risasi kilichokuwa kimefunika kile kikapu, kiliinuliwa na ndani ya kile kikapu alikuwako mwanamke ameketi!
And lo! a talent of leed was borun; and lo! a womman sittynge in myddil of the pot.
8 Akasema, “Huu ni uovu,” tena akamsukumia ndani ya kikapu na kushindilia kifuniko juu ya mdomo wa kikapu.
And he seide, This is vnpite, ether vnfeithfulnesse. And he castide doun hir in myddil of the pot, and sente a gobet of leed in to the mouth therof.
9 Kisha nikatazama juu: na pale mbele yangu, walikuwepo wanawake wawili, wakiwa na upepo katika mabawa yao! Walikuwa na mabawa kama ya korongo, nao wakainua kile kikapu na kuruka nacho kati ya mbingu na nchi.
And Y reiside myn iyen, and siy, and lo! twei wymmen goynge out, and a spirit in wyngis of hem; and thei hadden wyngis as wyngis of a kite, and reisiden the pot bitwixe heuene and erthe.
10 Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Wanakipeleka wapi hicho kikapu?”
And Y seide to the aungel that spak in me, Whidur beren these the pot?
11 Akanijibu, “Wanakipeleka katika nchi ya Babeli na kujenga nyumba kwa ajili yake. Itakapokuwa tayari, kikapu kitawekwa pale mahali pake.”
And he seide to me, That an hous be bildid therto in the lond of Sennaar, and be stablischid, and set there on his foundement.

< Zekaria 5 >