< Zekaria 3 >

1 Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, akiwa amesimama mbele ya malaika wa Bwana, naye Shetani amesimama upande wake wa kuume ili amshtaki.
Puis l'Éternel me fit voir Joshua, le grand sacrificateur, debout devant l'ange de l'Éternel, et Satan se tenait à sa droite, pour s'opposer à lui.
2 Bwana akamwambia Shetani, “Bwana akukemee Shetani! Bwana, ambaye ameichagua Yerusalemu, akukemee! Je, mtu huyu siyo kijinga kinachowaka kilichonyakuliwa kwenye moto?”
Et l'Éternel dit à Satan: Que l'Éternel te réprime, Satan! Que l'Éternel te réprime, lui qui a choisi Jérusalem! Celui-ci n'est-il pas un tison retiré du feu?
3 Wakati huu, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu alipokuwa amesimama mbele ya malaika.
Or Joshua était vêtu de vêtements sales, et se tenait devant l'ange.
4 Malaika akawaambia wale waliokuwa wamesimama mbele yake, “Mvueni hizo nguo zake chafu.” Kisha akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeiondoa dhambi yako, nami nitakuvika mavazi ya kitajiri.”
Et l'ange prit la parole, et dit à ceux qui se tenaient devant lui: Otez-lui ses vêtements sales. Puis il dit à Joshua: Vois, j'enlève ton iniquité, et je te revêts d'habits magnifiques.
5 Kisha nikasema, “Mvike kilemba kilicho safi kichwani mwake.” Kwa hiyo wakamvika kilemba safi kichwani na kumvika yale mavazi mengine, wakati malaika wa Bwana akiwa amesimama karibu.
Et je dis: Qu'on lui mette sur la tête une tiare pure! Et ils lui mirent sur la tête une tiare pure, et le revêtirent des vêtements, en présence de l'ange de l'Éternel.
6 Malaika wa Bwana akamwamuru Yoshua:
Puis l'ange de l'Éternel fit à Joshua cette déclaration:
7 “Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ikiwa utakwenda katika njia zangu na kushika masharti yangu, basi utaitawala nyumba yangu na kuwa na amri juu ya nyua zangu, nami nitakupa nafasi miongoni mwa hawa wasimamao hapa.
Ainsi a dit l'Éternel des armées: Si tu marches dans mes voies, et si tu gardes ce que je veux que l'on garde, tu jugeras aussi ma maison, tu garderas mes parvis, et je te donnerai libre accès parmi ceux-ci qui se tiennent devant moi.
8 “‘Sikiliza, ee Yoshua kuhani mkuu, pamoja na wenzako walioketi mbele yako, ambao ni watu walio ishara ya mambo yatakayokuja: Ninakwenda kumleta mtumishi wangu, Tawi.
Écoute, Joshua, grand sacrificateur, toi et tes compagnons qui sont assis devant toi; car se sont des hommes qui serviront de signes: voici, je vais faire venir mon serviteur, le Germe.
9 Tazama, jiwe nililoliweka mbele ya Yoshua! Kuna macho saba juu ya jiwe lile moja, nami nitachora maandishi juu yake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitaiondoa dhambi ya nchi hii kwa siku moja.
Car voici, quant à la pierre que j'ai mise devant Joshua, sur une seule pierre il y a sept yeux. Voici, je vais graver ce qui doit être gravé sur elle, dit l'Éternel des armées, et j'ôterai en un jour l'iniquité de ce pays.
10 “‘Katika siku hiyo kila mmoja wenu atamwalika jirani yake akae chini ya mzabibu wake na mtini wake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
En ce jour-là, dit l'Éternel des armées, vous vous appellerez l'un l'autre sous la vigne et sous le figuier.

< Zekaria 3 >