< Zekaria 3 >
1 Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, akiwa amesimama mbele ya malaika wa Bwana, naye Shetani amesimama upande wake wa kuume ili amshtaki.
and to see: see me [obj] Joshua [the] priest [the] great: large to stand: stand to/for face: before messenger: angel LORD and [the] Satan to stand: stand upon right his to/for to oppose him
2 Bwana akamwambia Shetani, “Bwana akukemee Shetani! Bwana, ambaye ameichagua Yerusalemu, akukemee! Je, mtu huyu siyo kijinga kinachowaka kilichonyakuliwa kwenye moto?”
and to say LORD to(wards) [the] Satan to rebuke LORD in/on/with you [the] Satan and to rebuke LORD in/on/with you [the] to choose in/on/with Jerusalem not this firebrand to rescue from fire
3 Wakati huu, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu alipokuwa amesimama mbele ya malaika.
and Joshua to be to clothe garment filthy and to stand: stand to/for face: before [the] messenger: angel
4 Malaika akawaambia wale waliokuwa wamesimama mbele yake, “Mvueni hizo nguo zake chafu.” Kisha akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeiondoa dhambi yako, nami nitakuvika mavazi ya kitajiri.”
and to answer and to say to(wards) [the] to stand: stand to/for face: before his to/for to say to turn aside: remove [the] garment [the] filthy from upon him and to say to(wards) him to see: behold! to pass: bring from upon you iniquity: crime your and to clothe [obj] you robe
5 Kisha nikasema, “Mvike kilemba kilicho safi kichwani mwake.” Kwa hiyo wakamvika kilemba safi kichwani na kumvika yale mavazi mengine, wakati malaika wa Bwana akiwa amesimama karibu.
and to say to set: put turban pure upon head his and to set: put [the] turban [the] pure upon head his and to clothe him garment and messenger: angel LORD to stand: stand
6 Malaika wa Bwana akamwamuru Yoshua:
and to testify messenger: angel LORD in/on/with Joshua to/for to say
7 “Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ikiwa utakwenda katika njia zangu na kushika masharti yangu, basi utaitawala nyumba yangu na kuwa na amri juu ya nyua zangu, nami nitakupa nafasi miongoni mwa hawa wasimamao hapa.
thus to say LORD Hosts if in/on/with way: conduct my to go: walk and if [obj] charge my to keep: obey and also you(m. s.) to judge [obj] house: home my and also to keep: guard [obj] court my and to give: give to/for you journey between [the] to stand: stand [the] these
8 “‘Sikiliza, ee Yoshua kuhani mkuu, pamoja na wenzako walioketi mbele yako, ambao ni watu walio ishara ya mambo yatakayokuja: Ninakwenda kumleta mtumishi wangu, Tawi.
to hear: hear please Joshua [the] priest [the] great: large you(m. s.) and neighbor your [the] to dwell to/for face: before your for human wonder they(masc.) for look! I to come (in): bring [obj] servant/slave my branch
9 Tazama, jiwe nililoliweka mbele ya Yoshua! Kuna macho saba juu ya jiwe lile moja, nami nitachora maandishi juu yake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitaiondoa dhambi ya nchi hii kwa siku moja.
for behold [the] stone which to give: put to/for face: before Joshua upon stone one seven eye look! I to engrave engraving her utterance LORD Hosts and to remove [obj] iniquity: crime [the] land: country/planet [the] he/she/it in/on/with day one
10 “‘Katika siku hiyo kila mmoja wenu atamwalika jirani yake akae chini ya mzabibu wake na mtini wake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
in/on/with day [the] he/she/it utterance LORD Hosts to call: call to man: anyone to/for neighbor his to(wards) underneath: under vine and to(wards) underneath: under fig