< Zekaria 3 >

1 Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, akiwa amesimama mbele ya malaika wa Bwana, naye Shetani amesimama upande wake wa kuume ili amshtaki.
And he showed me Joshua, the high-priest, standing before the angel of Jehovah, and the adversary standing at his right hand, to accuse him.
2 Bwana akamwambia Shetani, “Bwana akukemee Shetani! Bwana, ambaye ameichagua Yerusalemu, akukemee! Je, mtu huyu siyo kijinga kinachowaka kilichonyakuliwa kwenye moto?”
And Jehovah said to the adversary: — Jehovah rebuke thee, thou adversary, Even Jehovah, who hath chosen Jerusalem, rebuke thee! Is not this man a brand plucked out of the fire?
3 Wakati huu, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu alipokuwa amesimama mbele ya malaika.
Now Joshua was clothed with filthy garments, and stood before the angel.
4 Malaika akawaambia wale waliokuwa wamesimama mbele yake, “Mvueni hizo nguo zake chafu.” Kisha akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeiondoa dhambi yako, nami nitakuvika mavazi ya kitajiri.”
And he [[the angel]] spake and said to them [[the angels]] that stood before him, saying, Take off the filthy garments from him. And to him he said, Behold, I have caused thine iniquity to pass from thee, and will clothe thee with goodly apparel.
5 Kisha nikasema, “Mvike kilemba kilicho safi kichwani mwake.” Kwa hiyo wakamvika kilemba safi kichwani na kumvika yale mavazi mengine, wakati malaika wa Bwana akiwa amesimama karibu.
And I said, Let them set a fair mitre upon his head! And they set a fair mitre upon his head, and clothed him with garments. And the angel of Jehovah stood by.
6 Malaika wa Bwana akamwamuru Yoshua:
And the angel of Jehovah declared to Joshua and said:
7 “Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ikiwa utakwenda katika njia zangu na kushika masharti yangu, basi utaitawala nyumba yangu na kuwa na amri juu ya nyua zangu, nami nitakupa nafasi miongoni mwa hawa wasimamao hapa.
Thus saith Jehovah of hosts: If thou wilt walk in my ways, And if thou wilt keep my charge, Then thou shalt also rule my house, And shalt also keep my courts, And I will give thee guides among these that stand by.
8 “‘Sikiliza, ee Yoshua kuhani mkuu, pamoja na wenzako walioketi mbele yako, ambao ni watu walio ishara ya mambo yatakayokuja: Ninakwenda kumleta mtumishi wangu, Tawi.
Hear now, O Joshua, high-priest, Thou and thy companions, who sit before thee! For they are men that are signs. For, behold, I will cause to come my servant, the Branch.
9 Tazama, jiwe nililoliweka mbele ya Yoshua! Kuna macho saba juu ya jiwe lile moja, nami nitachora maandishi juu yake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitaiondoa dhambi ya nchi hii kwa siku moja.
For, behold, the stone which I have laid before Joshua, Upon this one stone shall be seven eyes; Behold, I will engrave the graving thereof, saith Jehovah of hosts; And I will remove the iniquity of this land in one day.
10 “‘Katika siku hiyo kila mmoja wenu atamwalika jirani yake akae chini ya mzabibu wake na mtini wake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
In that day, saith Jehovah of hosts, Shall ye invite every one his neighbor Under the vine and under the fig-tree.

< Zekaria 3 >