< Zekaria 2 >
1 Kisha nikatazama juu: pale mbele yangu alikuwepo mtu mwenye kamba ya kupimia mkononi mwake!
Es atkal pacēlu savas acis un skatījos, un redzi, tur bija vīrs, un viņa rokā mēra aukla.
2 Nikamuuliza, “Unakwenda wapi?” Akanijibu, “Kupima Yerusalemu, kupata urefu na upana wake.”
Un es sacīju: kurp iedams? Un viņš sacīja uz mani: Jeruzālemi mērot un lūkot, kāds viņas platums un kāds viņas garums.
3 Kisha malaika aliyekuwa akizungumza nami akaondoka, malaika mwingine akaja kukutana naye
Un redzi, tas eņģelis, kas ar mani runāja, izgāja ārā. Un viens cits eņģelis tam nāca pretī.
4 na kumwambia: “Kimbia, umwambie yule kijana, ‘Yerusalemu utakuwa mji usio na kuta kwa sababu ya wingi wa watu na mifugo iliyomo.
Un viņš uz to sacīja: teci, runā uz šo jaunekli un saki: Jeruzālemē dzīvos bez mūriem aiz liela cilvēku un lopu pulka viņas vidu.
5 Mimi mwenyewe nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka,’ asema Bwana, ‘nami nitakuwa utukufu wake ndani yake.’
Un Es, saka Tas Kungs, viņai būšu par degošu mūri visapkārt, un Es būšu par godību viņas vidū.
6 “Njooni! Njooni! Kimbieni mtoke katika nchi ya kaskazini,” asema Bwana, “Kwa kuwa nimewatawanya kwenye pande nne za mbingu,” asema Bwana.
Vai, vai, bēdziet jel no ziemeļa zemes! saka Tas Kungs; jo Es jūs izpletīšu uz tiem četriem debess vējiem, saka Tas Kungs.
7 “Njoo, ee Sayuni! Kimbia, wewe ukaaye ndani ya Binti Babeli!”
Vai, Ciāna, glābies, tu, kas dzīvo pie Bābeles meitas.
8 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Baada ya yeye kuniheshimu na kunituma mimi dhidi ya mataifa yaliyokuteka nyara, kwa kuwa yeyote awagusaye ninyi, anaigusa mboni ya jicho lake,
Jo tā saka Tas Kungs Cebaot: pēc godības Viņš mani sūtījis pie tiem pagāniem, kas jūs aplaupījuši; jo kas jūs aizskar, tas aizskar Viņa acs raugu.
9 hakika nitauinua mkono wangu dhidi yao ili watumwa wao wawateke nyara. Ndipo mtakapojua ya kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma.
Jo redzi, Es cilāšu Savu roku pār tiem; tie būs par laupījumu saviem kalpiem; tā jūs samanīsiet, ka Tas Kungs Cebaot mani sūtījis.
10 “Piga kelele na ufurahie, ee Binti Sayuni, kwa maana ninakuja, nami nitaishi miongoni mwenu,” asema Bwana.
Gavilē un priecājies, Ciānas meita, jo redzi, Es nāku un dzīvošu tavā vidū, saka Tas Kungs;
11 “Mataifa mengi yataunganishwa na Bwana siku hiyo, nao watakuwa watu wangu. Nitaishi miongoni mwenu nanyi mtajua kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma kwenu.
Un daudz pagāni tai dienā piebiedrosies Tam Kungam, un tie Man būs par ļaudīm, un Es dzīvošu tavā vidū, un tu samanīsi, ka Tas Kungs Cebaot mani pie tevis sūtījis.
12 Bwana atairithi Yuda kama fungu lake katika nchi takatifu na atachagua tena Yerusalemu.
Tad Tas Kungs iemantos Jūdu par Savu tiesu tai svētā zemē un izredzēs atkal Jeruzālemi.
13 Tulieni mbele za Bwana, enyi watu wote, kwa sababu ameinuka kutoka makao yake matakatifu.”
Ciet klusu, visa miesa, Tā Kunga priekšā! Jo Viņš ir uzcēlies no Savas svētās vietas.