< Zekaria 2 >
1 Kisha nikatazama juu: pale mbele yangu alikuwepo mtu mwenye kamba ya kupimia mkononi mwake!
Then I looked up and saw a man with a measuring line in his hand.
2 Nikamuuliza, “Unakwenda wapi?” Akanijibu, “Kupima Yerusalemu, kupata urefu na upana wake.”
I said, ‘Where are you going?’ He replied, ‘To measure Jerusalem, to see what is its breadth and length.’
3 Kisha malaika aliyekuwa akizungumza nami akaondoka, malaika mwingine akaja kukutana naye
Then the messenger who talked with me stepped forward, and another messenger went out to meet him,
4 na kumwambia: “Kimbia, umwambie yule kijana, ‘Yerusalemu utakuwa mji usio na kuta kwa sababu ya wingi wa watu na mifugo iliyomo.
and said to him, ‘Run and tell to that young man that Jerusalem will be inhabited like a village without walls, because so many people and cattle will live there.
5 Mimi mwenyewe nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka,’ asema Bwana, ‘nami nitakuwa utukufu wake ndani yake.’
For I, says the Lord, will be a wall of fire her, and I will be the glory in the midst of her.
6 “Njooni! Njooni! Kimbieni mtoke katika nchi ya kaskazini,” asema Bwana, “Kwa kuwa nimewatawanya kwenye pande nne za mbingu,” asema Bwana.
Up! Away! Flee from the land of the north, says the Lord. For I have spread you abroad as the four winds of the heavens, says the Lord.
7 “Njoo, ee Sayuni! Kimbia, wewe ukaaye ndani ya Binti Babeli!”
Up, escape to Zion, you who live in Babylon.
8 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Baada ya yeye kuniheshimu na kunituma mimi dhidi ya mataifa yaliyokuteka nyara, kwa kuwa yeyote awagusaye ninyi, anaigusa mboni ya jicho lake,
This is what the Lord of hosts says to the nations which plundered you: Whoever touches you touches the apple of my eye.
9 hakika nitauinua mkono wangu dhidi yao ili watumwa wao wawateke nyara. Ndipo mtakapojua ya kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma.
I will raise my hand against them. They will be plunder for their own slaves; and you will know that the Lord of hosts has sent me.
10 “Piga kelele na ufurahie, ee Binti Sayuni, kwa maana ninakuja, nami nitaishi miongoni mwenu,” asema Bwana.
‘Sing and rejoice, daughter of Zion! I am coming, I will live among you, says the Lord.
11 “Mataifa mengi yataunganishwa na Bwana siku hiyo, nao watakuwa watu wangu. Nitaishi miongoni mwenu nanyi mtajua kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma kwenu.
Many nations will join themselves to the Lord in that day, and will be his people, and he will live among you. You will know that the Lord of hosts has sent me to you.
12 Bwana atairithi Yuda kama fungu lake katika nchi takatifu na atachagua tena Yerusalemu.
The Lord will inherit Judah as his portion in the holy land. He will again choose Jerusalem.
13 Tulieni mbele za Bwana, enyi watu wote, kwa sababu ameinuka kutoka makao yake matakatifu.”
Be silent, everyone, in the presence of the Lord, because he is coming from his holy dwelling.’