< Zekaria 2 >
1 Kisha nikatazama juu: pale mbele yangu alikuwepo mtu mwenye kamba ya kupimia mkononi mwake!
And I lifted up my eyes, and I saw, and behold, a man, and in his hand was a measuring line.
2 Nikamuuliza, “Unakwenda wapi?” Akanijibu, “Kupima Yerusalemu, kupata urefu na upana wake.”
And I said, “Where are you going?” And he said to me, “To measure Jerusalem, so that I may see how great its width and how great its length may be.”
3 Kisha malaika aliyekuwa akizungumza nami akaondoka, malaika mwingine akaja kukutana naye
And behold, the angel, who had been speaking with me, departed, and another angel went out to meet him.
4 na kumwambia: “Kimbia, umwambie yule kijana, ‘Yerusalemu utakuwa mji usio na kuta kwa sababu ya wingi wa watu na mifugo iliyomo.
And he said to him: Hurry, speak to this young man, saying: Jerusalem will be inhabited without walls, because of the multitude of men and beasts of burden in its midst.
5 Mimi mwenyewe nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka,’ asema Bwana, ‘nami nitakuwa utukufu wake ndani yake.’
And I will be to it, says the Lord, a wall of fire all around. And in glory, I will be in its midst.
6 “Njooni! Njooni! Kimbieni mtoke katika nchi ya kaskazini,” asema Bwana, “Kwa kuwa nimewatawanya kwenye pande nne za mbingu,” asema Bwana.
O, O flee from the land of the North, says the Lord, for I have scattered you into the four winds of heaven, says the Lord.
7 “Njoo, ee Sayuni! Kimbia, wewe ukaaye ndani ya Binti Babeli!”
O Zion, flee, you who dwell with the daughter of Babylon.
8 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Baada ya yeye kuniheshimu na kunituma mimi dhidi ya mataifa yaliyokuteka nyara, kwa kuwa yeyote awagusaye ninyi, anaigusa mboni ya jicho lake,
For thus says the Lord of hosts: After the glory, he has sent me to the Gentiles, which have despoiled you. For he who touches you, touches the pupil of my eye.
9 hakika nitauinua mkono wangu dhidi yao ili watumwa wao wawateke nyara. Ndipo mtakapojua ya kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma.
For behold, I lift up my hand over them, and they will be a prey to those who had served them. And you will know that the Lord of hosts has sent me.
10 “Piga kelele na ufurahie, ee Binti Sayuni, kwa maana ninakuja, nami nitaishi miongoni mwenu,” asema Bwana.
Sing praise and rejoice, daughter of Zion. For behold, I approach, and I will dwell in your midst, says the Lord.
11 “Mataifa mengi yataunganishwa na Bwana siku hiyo, nao watakuwa watu wangu. Nitaishi miongoni mwenu nanyi mtajua kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma kwenu.
And many nations will be joined to the Lord in that day, and they will be my people, and I will dwell in your midst. And you will know that the Lord of hosts has sent me to you.
12 Bwana atairithi Yuda kama fungu lake katika nchi takatifu na atachagua tena Yerusalemu.
And the Lord will possess his portion, Judah, in the sanctified land, and still he will single out Jerusalem.
13 Tulieni mbele za Bwana, enyi watu wote, kwa sababu ameinuka kutoka makao yake matakatifu.”
Let all flesh be silent before the face of the Lord: for he has arisen from his holy dwelling place.