< Zekaria 2 >
1 Kisha nikatazama juu: pale mbele yangu alikuwepo mtu mwenye kamba ya kupimia mkononi mwake!
And I lifted up mine eyes, and looked, and behold a man, and in his hand a measuring line.
2 Nikamuuliza, “Unakwenda wapi?” Akanijibu, “Kupima Yerusalemu, kupata urefu na upana wake.”
And I said to him, Whither goest thou? And he said to me, To measure Jerusalem, to see what is the breadth of it, and what is the length of it.
3 Kisha malaika aliyekuwa akizungumza nami akaondoka, malaika mwingine akaja kukutana naye
And, behold, the angel that spoke with me stood [by], and another angel went forth to meet him,
4 na kumwambia: “Kimbia, umwambie yule kijana, ‘Yerusalemu utakuwa mji usio na kuta kwa sababu ya wingi wa watu na mifugo iliyomo.
and spoke to him, saying, Run and speak to that young man, saying, Jerusalem shall be fully inhabited by reason of the abundance of men and cattle in the midst of her.
5 Mimi mwenyewe nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka,’ asema Bwana, ‘nami nitakuwa utukufu wake ndani yake.’
And I will be to her, saith the Lord, a wall of fire round about, and I will be for a glory in the midst of her.
6 “Njooni! Njooni! Kimbieni mtoke katika nchi ya kaskazini,” asema Bwana, “Kwa kuwa nimewatawanya kwenye pande nne za mbingu,” asema Bwana.
Ho, ho, flee from the land of the north, saith the Lord: for I will gather you from the four winds of heaven, saith the Lord,
7 “Njoo, ee Sayuni! Kimbia, wewe ukaaye ndani ya Binti Babeli!”
[even] to Sion: deliver yourselves, ye that dwell [with] the daughter of Babylon.
8 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Baada ya yeye kuniheshimu na kunituma mimi dhidi ya mataifa yaliyokuteka nyara, kwa kuwa yeyote awagusaye ninyi, anaigusa mboni ya jicho lake,
For thus saith the Lord Almighty; After the glory has he sent me to the nations that spoiled you: for he that touches you is as one that touches the apple of his eye.
9 hakika nitauinua mkono wangu dhidi yao ili watumwa wao wawateke nyara. Ndipo mtakapojua ya kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma.
For, behold, I bring my hand upon them, and they shall be a spoil to them that serve them: and ye shall know that the Lord Almighty has sent me.
10 “Piga kelele na ufurahie, ee Binti Sayuni, kwa maana ninakuja, nami nitaishi miongoni mwenu,” asema Bwana.
Rejoice and be glad, O daughter of Sion: for, behold, I come, and will dwell in the midst of thee, saith the Lord.
11 “Mataifa mengi yataunganishwa na Bwana siku hiyo, nao watakuwa watu wangu. Nitaishi miongoni mwenu nanyi mtajua kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma kwenu.
And many nations shall flee for refuge to the Lord in that day, and they shall be for a people to him, and they shall dwell in the midst of thee: and thou shalt know that the Lord Almighty has sent me to thee.
12 Bwana atairithi Yuda kama fungu lake katika nchi takatifu na atachagua tena Yerusalemu.
And the Lord shall inherit Juda his portion in the holy [land], and he will yet choose Jerusalem.
13 Tulieni mbele za Bwana, enyi watu wote, kwa sababu ameinuka kutoka makao yake matakatifu.”
Let all flesh fear before the Lord: for he has risen up from his holy clouds.