< Zekaria 14 >

1 Siku ya Bwana inakuja ambayo nyara zilizotekwa kwenu zitagawanywa miongoni mwenu.
Lo! daies comen, seith the Lord, and thi spuylis schulen be departid in the myddil of thee.
2 Nitayakusanya mataifa yote huko Yerusalemu kupigana dhidi yake, mji utatekwa, nyumba zitavamiwa na kuporwa na wanawake watanajisiwa. Nusu ya mji watakwenda uhamishoni, lakini watakaobaki hawataondolewa kutoka mjini.
And Y schal gadere alle folkis to Jerusalem, in to batel; and the citee schal be takun, and housis schulen be distried, and wymmen schulen be defoulid. And the myddil part of the citee schal go out in to caitiftee, and the `tother part of the puple schal not be takun awei fro the citee.
3 Kisha Bwana atatoka na kupigana dhidi ya watu wa yale mataifa, kama apiganavyo siku ya vita.
And the Lord schal go out, and schal fiyte ayens tho folkis, as he fauyte in the dai of strijf.
4 Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, mashariki mwa Yerusalemu, nao Mlima wa Mizeituni utagawanyika mara mbili kuanzia mashariki hadi magharibi, ukifanya bonde kubwa, nusu ya mlima ukisogea kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
And hise feet schulen stonde in that dai on the hil of olyues, that is ayens Jerusalem at the eest. And the hil of olyues schal be coruun of the myddil part therof to the eest and to the west, bi ful greet biforbrekyng; and the myddil of the hil schal be departid to the north, and the myddil therof to the south.
5 Nanyi mtakimbia kupitia katika bonde hilo la mlima wangu kwa kuwa litaenea hadi Aseli. Mtakimbia kama mlivyokimbia tetemeko la ardhi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda. Kisha Bwana Mungu wangu atakuja na watakatifu wote pamoja naye.
And ye schulen fle to the valei of myn hillis, for the valei of hillis schal be ioyned togidere til to the nexte. And ye schulen fle, as ye fledden fro the face of erthe mouyng in the daies of Osie, kyng of Juda; and my Lord God schal come, and alle seyntis with hym.
6 Siku hiyo hakutakuwepo nuru, baridi wala theluji.
And it schal be, in that dai liyt schal not be, but coold and frost.
7 Itakuwa siku ya kipekee, isiyo na mchana wala usiku, siku ijulikanayo na Bwana. Jioni inapofika nuru itakuwepo.
And `ther schal be o dai, which is knowun to the Lord, not day, nether niyt, and in tyme of euentid liyt schal be.
8 Siku hiyo, maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu, nusu kwenda kwenye bahari ya mashariki, na nusu kwenda kwenye bahari ya magharibi wakati wa kiangazi na wakati wa masika.
And it schal be, in that dai quyke watris schulen go out of Jerusalem, the myddil of hem schal go out to the eest see, and the myddil of hem to the laste see; in somer and in wynter thei schulen be.
9 Bwana atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo atakuwepo Bwana mmoja na jina lake litakuwa jina pekee.
And the Lord schal be kyng on al erthe; in that dai there schal be o Lord, and his name schal be oon.
10 Nchi yote kuanzia Geba, kaskazini mwa Yuda, hadi Rimoni, kusini mwa Yerusalemu, itakuwa kama Araba. Lakini Yerusalemu utainuliwa juu na kubaki mahali pake, toka Lango la Benyamini hadi mahali pa Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni na kutoka Mnara wa Hananeli hadi kwenye mashinikizo ya divai ya mfalme.
And al erthe schal turne ayen til to desert, fro the litil hil Remmon to the south of Jerusalem. And it schal be reisid, and schal dwelle in his place, fro the yate of Beniamyn til to place of the formere yate, and til to the yate of the corneris, and fro the tour of Ananyel til to the pressouris of the kyng.
11 Utakaliwa na watu, kamwe hautaharibiwa tena, Yerusalemu utakaa salama.
And thei schulen dwelle there ynne, and cursidnesse schal no more be, but Jerusalem schal sitte sikir.
12 Hii ndiyo tauni ambayo Bwana atapiga nayo mataifa yote ambayo yalipigana dhidi ya Yerusalemu: Nyama ya miili yao itaoza wangali wamesimama kwa miguu yao, macho yao yataoza kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza vinywani mwao.
And this schal be the wounde, bi which the Lord schal smyte alle folkis, that fouyten ayens Jerusalem; the fleisch of ech man stondynge on hise feet schal faile, and hise iyen schulen faile togidere in her hoolis, and her tunge schal faile togidere in her mouth.
13 Katika siku hiyo Bwana atawatia wanaume hofu kuu. Kila mwanaume atakamata mkono wa mwenzake nao watashambuliana.
In that dai greet noise of the Lord schal be in hem, and a man schal catche the hond of his neiybore; and his hond schal be lockid togidere on hond of his neiybore.
14 Yuda pia atapigana katika Yerusalemu. Utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka Yerusalemu utakusanywa, wingi wa dhahabu, fedha na nguo.
But and Judas schal fiyte ayens Jerusalem; and richessis of alle folkis in cumpas schulen be gaderide togidere, gold, and siluer, and many clothis ynow.
15 Tauni ya aina iyo hiyo itapiga farasi na nyumbu, ngamia na punda, nao wanyama wote walioko kwenye kambi za adui.
And so fallyng schal be of hors, and mule, and camel, and asse, and of alle werk beestis, that weren in tho castels, as this fallyng.
16 Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
And alle that schulen be residue of alle folkis, that camen ayens Jerusalem, schulen stie vp fro yeer in to yeer, that thei worschipe the kyng, Lord of oostis, and halewe the feeste of tabernaclis.
17 Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao.
And it schal be, reyn schal not be on hem that schulen not stie vp of the meyneis of erthe to Jerusalem, `that thei worschipe the king, Lord of oostis.
18 Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. Bwana ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
`That and if the meynee of Egipt schal not stie vp, and schal not come, nether on hem schal be reyn; but fallyng schal be, bi which the Lord schal smyte alle folkis, whiche stieden not, for to halewe the feeste of tabernaclis.
19 Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
This schal be the synne of Egipt, and this the synne of alle folkis, that stieden not, for to halewe the feeste of tabernaclis.
20 Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: Takatifu kwa Bwana, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya Bwana vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu.
In that dai, that that is on the bridil of hors schal be hooli to the Lord; and caudruns schulen be in the hous of the Lord, as cruetis bifor the auter.
21 Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And euery caudrun in Jerusalem and Juda schal be halewid to the Lord of oostis. And alle men schulen come offrynge, and schulen take of tho, and schulen sethe in tho; and a marchaunt schal no more be in the hous of the Lord of oostis in that day.

< Zekaria 14 >