< Zekaria 14 >

1 Siku ya Bwana inakuja ambayo nyara zilizotekwa kwenu zitagawanywa miongoni mwenu.
A day is coming for the Lord, when your plundered possessions will be divided while you watch.
2 Nitayakusanya mataifa yote huko Yerusalemu kupigana dhidi yake, mji utatekwa, nyumba zitavamiwa na kuporwa na wanawake watanajisiwa. Nusu ya mji watakwenda uhamishoni, lakini watakaobaki hawataondolewa kutoka mjini.
And all the nations will gather to Jerusalem, to fight against it. The city will be taken and the houses plundered and the women raped. Half of the city will go into captivity, and the rest of the people left in the ruins.
3 Kisha Bwana atatoka na kupigana dhidi ya watu wa yale mataifa, kama apiganavyo siku ya vita.
Then the Lord will go forth and fight against these nations, as once he fought in the day of battle.
4 Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, mashariki mwa Yerusalemu, nao Mlima wa Mizeituni utagawanyika mara mbili kuanzia mashariki hadi magharibi, ukifanya bonde kubwa, nusu ya mlima ukisogea kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
On that day his feet will stand on the Mount of Olives, (which is opposite Jerusalem, on the east). The Mount of Olives will be split into halves, from east to west, by an exceedingly great valley; and half of the mountain will slide northwards and half southwards.
5 Nanyi mtakimbia kupitia katika bonde hilo la mlima wangu kwa kuwa litaenea hadi Aseli. Mtakimbia kama mlivyokimbia tetemeko la ardhi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda. Kisha Bwana Mungu wangu atakuja na watakatifu wote pamoja naye.
You will escape through my valley – the valley between the hills will extend as far as Azel, and you will flee as you fled from before the earthquake, in the days of Uzziah king of Judah. But the Lord your God will come, and all the holy ones with him.
6 Siku hiyo hakutakuwepo nuru, baridi wala theluji.
And in that day, there will be no heat nor cold nor frost,
7 Itakuwa siku ya kipekee, isiyo na mchana wala usiku, siku ijulikanayo na Bwana. Jioni inapofika nuru itakuwepo.
but it will be constant day – it is known to the Lord – with neither day nor night. Even at evening time there will be light.
8 Siku hiyo, maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu, nusu kwenda kwenye bahari ya mashariki, na nusu kwenda kwenye bahari ya magharibi wakati wa kiangazi na wakati wa masika.
And on that day living waters will flow from Jerusalem, half of them to the eastern sea and half of them to the western sea; in both summer and winter.
9 Bwana atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo atakuwepo Bwana mmoja na jina lake litakuwa jina pekee.
The Lord will be king over all the earth. On that day the Lord will be one, and his name one.
10 Nchi yote kuanzia Geba, kaskazini mwa Yuda, hadi Rimoni, kusini mwa Yerusalemu, itakuwa kama Araba. Lakini Yerusalemu utainuliwa juu na kubaki mahali pake, toka Lango la Benyamini hadi mahali pa Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni na kutoka Mnara wa Hananeli hadi kwenye mashinikizo ya divai ya mfalme.
The land will be changed to plain, from Geba to Rimmon, south of Jerusalem, but Jerusalem will be high and inhabited as it stands, from the Benjamin Gate up to the place of the first gate, and from the Tower of Hananel to the Corner Gate, and as far as the king’s winepresses.
11 Utakaliwa na watu, kamwe hautaharibiwa tena, Yerusalemu utakaa salama.
Jerusalem will be inhabited, for never again will it be doomed to destruction, and its people will abide in security.
12 Hii ndiyo tauni ambayo Bwana atapiga nayo mataifa yote ambayo yalipigana dhidi ya Yerusalemu: Nyama ya miili yao itaoza wangali wamesimama kwa miguu yao, macho yao yataoza kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza vinywani mwao.
This is the plague with which the Lord will strike all the peoples who array themselves against Jerusalem: he will make their flesh rot while they stand on their feet, and their eyes will rot in their sockets, and their tongues will rot in their mouth.
13 Katika siku hiyo Bwana atawatia wanaume hofu kuu. Kila mwanaume atakamata mkono wa mwenzake nao watashambuliana.
On that day a great panic sent by the Lord will fall on them. Everyone will seize their neighbours and attack them.
14 Yuda pia atapigana katika Yerusalemu. Utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka Yerusalemu utakusanywa, wingi wa dhahabu, fedha na nguo.
Even Judah will fight at Jerusalem, and the wealth of the surrounding nations will be gathered up – gold and silver and piles of clothing.
15 Tauni ya aina iyo hiyo itapiga farasi na nyumbu, ngamia na punda, nao wanyama wote walioko kwenye kambi za adui.
Plague will fall upon the horses, mules, camels, and asses, and on all the animals in all those camps.
16 Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
All who are left of all the nations which fought against Jerusalem will come up from year to year to worship the King, the Lord of hosts, and to keep the pilgrim-feast of tabernacles.
17 Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao.
Whoever of all the peoples of the earth will not come up to Jerusalem to worship the King, the Lord of hosts, on them there will be no rain.
18 Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. Bwana ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
If the family of Egypt does not go up nor enter in, on them also will come the plague with which the Lord will strike the nations.
19 Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
This will be the punishment for the sin of Egypt and the punishment for the sin of all nations which do not come up to keep the feast of the tabernacles.
20 Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: Takatifu kwa Bwana, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya Bwana vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu.
On that day there will be inscribed upon the bells of the horses, ‘Holy to the Lord’ and the pots in the house of the Lord will be as holy as the sacrificial bowls before the altars.
21 Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Every pot in Jerusalem and in Judah will be holy to the Lord of hosts and all who sacrifice will come and take of them and cook the sacrifices in them. There will be no more traffickers in the house of the Lord of hosts in that day.

< Zekaria 14 >