< Zekaria 14 >
1 Siku ya Bwana inakuja ambayo nyara zilizotekwa kwenu zitagawanywa miongoni mwenu.
Behold, the day of Jehovah cometh, When thy spoil shall be divided in the midst of thee.
2 Nitayakusanya mataifa yote huko Yerusalemu kupigana dhidi yake, mji utatekwa, nyumba zitavamiwa na kuporwa na wanawake watanajisiwa. Nusu ya mji watakwenda uhamishoni, lakini watakaobaki hawataondolewa kutoka mjini.
For I will gather all nations against Jerusalem to battle; And the city shall be taken, And the houses shall be rifled, And the women shall be ravished; And half of the city shall go forth into captivity, And the residue of the people shall not be cut off from the city.
3 Kisha Bwana atatoka na kupigana dhidi ya watu wa yale mataifa, kama apiganavyo siku ya vita.
Then shall Jehovah go forth, And fight against those nations, As he once fought in the day of battle.
4 Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, mashariki mwa Yerusalemu, nao Mlima wa Mizeituni utagawanyika mara mbili kuanzia mashariki hadi magharibi, ukifanya bonde kubwa, nusu ya mlima ukisogea kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
And his feet shall stand in that day upon the Mount of Olives, Which is before Jerusalem on the east; And the Mount of Olives shall be cloven in the middle of it, eastward and westward, Into a very great valley; And half of the mountain shall remove toward the north, And half of it toward the south.
5 Nanyi mtakimbia kupitia katika bonde hilo la mlima wangu kwa kuwa litaenea hadi Aseli. Mtakimbia kama mlivyokimbia tetemeko la ardhi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda. Kisha Bwana Mungu wangu atakuja na watakatifu wote pamoja naye.
And ye shall flee through the valley of my mountains, For the valley of the mountains shall reach to Azal; Yea, ye shall flee, as ye fled before the earthquake In the days of Uzziah, king of Judah. And Jehovah, my God, will come, And all his holy ones with him.
6 Siku hiyo hakutakuwepo nuru, baridi wala theluji.
And it shall come to pass in that day That there shall he no light, but cold and ice;
7 Itakuwa siku ya kipekee, isiyo na mchana wala usiku, siku ijulikanayo na Bwana. Jioni inapofika nuru itakuwepo.
And there shall be one day, (Known to Jehovah is it, ) It shall be neither day nor night; But at the time of evening there shall be light.
8 Siku hiyo, maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu, nusu kwenda kwenye bahari ya mashariki, na nusu kwenda kwenye bahari ya magharibi wakati wa kiangazi na wakati wa masika.
And it shall come to pass in that day That living waters shall go out from Jerusalem, Half of them toward the eastern sea, And half of them toward the western sea; In summer and in winter shall they be.
9 Bwana atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo atakuwepo Bwana mmoja na jina lake litakuwa jina pekee.
And Jehovah shall be king over all the earth; In that day shall Jehovah be one, and his name one.
10 Nchi yote kuanzia Geba, kaskazini mwa Yuda, hadi Rimoni, kusini mwa Yerusalemu, itakuwa kama Araba. Lakini Yerusalemu utainuliwa juu na kubaki mahali pake, toka Lango la Benyamini hadi mahali pa Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni na kutoka Mnara wa Hananeli hadi kwenye mashinikizo ya divai ya mfalme.
The whole land shall be turned into a plain, From Geba to Rimmon, south of Jerusalem; And the city shall be exalted and inhabited in her place, From the gate of Benjamin to the place of the former gate, And to the corner gate, And from the tower of Hananeel to the king's wine-presses.
11 Utakaliwa na watu, kamwe hautaharibiwa tena, Yerusalemu utakaa salama.
Men shall dwell therein, And there shall be no more destruction; But Jerusalem shall dwell securely.
12 Hii ndiyo tauni ambayo Bwana atapiga nayo mataifa yote ambayo yalipigana dhidi ya Yerusalemu: Nyama ya miili yao itaoza wangali wamesimama kwa miguu yao, macho yao yataoza kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza vinywani mwao.
And this shall be the plague With which Jehovah will smite all the nations Which warred against Jerusalem: Their flesh shall consume away while they stand upon their feet, And their eyes shall consume away in their sockets, And their tongue shall consume away in their mouth.
13 Katika siku hiyo Bwana atawatia wanaume hofu kuu. Kila mwanaume atakamata mkono wa mwenzake nao watashambuliana.
And it shall come to pass in that day, That there shall be a great tumult among them from Jehovah; And they shall lay hold every one on the hand of his neighbor, And his hand shall rise up against the hand of his neighbor.
14 Yuda pia atapigana katika Yerusalemu. Utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka Yerusalemu utakusanywa, wingi wa dhahabu, fedha na nguo.
And Judah also shall fight against Jerusalem; But the wealth of all the nations round about shall be gathered together, Gold and silver and apparel in great abundance.
15 Tauni ya aina iyo hiyo itapiga farasi na nyumbu, ngamia na punda, nao wanyama wote walioko kwenye kambi za adui.
And so shall be the plague of the horse, Of the mule, of the camel, and of the ass, And of every beast which shall be in those camps, Even as this plague.
16 Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
And it shall be, that every one that is left Of all the nations which come against Jerusalem, Even they shall go up, from year to year, To worship the King, Jehovah of hosts, And to keep the feast of tabernacles.
17 Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao.
And it shall be that whoso will not go up, Of the families of the earth, to Jerusalem, To worship the King, Jehovah of hosts, Upon them shall be no rain.
18 Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. Bwana ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
And if the family of Egypt go not up, and come not, Then not for them shall there be water. The plague shall come upon them With which Jehovah shall smite the nations Which go not up to keep the feast of tabernacles.
19 Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
This shall be the punishment of Egypt, And the punishment of all the nations That come not up to keep the feast of tabernacles.
20 Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: Takatifu kwa Bwana, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya Bwana vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu.
In that day, upon the bells of the horses Shall be written, “Holy to Jehovah.” And the pots in the house of Jehovah Shall be as the bowls before the altar.
21 Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And every pot in Jerusalem and in Judah Shall be holy to Jehovah of hosts; And all that sacrifice shall come, And shall take of them, and seethe therein. And there shall be no more a trader In the house of Jehovah of hosts, in that day.