< Zekaria 14 >

1 Siku ya Bwana inakuja ambayo nyara zilizotekwa kwenu zitagawanywa miongoni mwenu.
Se, en Dag kommer, HERRENS Dag, da dit Bytte skal deles i dig.
2 Nitayakusanya mataifa yote huko Yerusalemu kupigana dhidi yake, mji utatekwa, nyumba zitavamiwa na kuporwa na wanawake watanajisiwa. Nusu ya mji watakwenda uhamishoni, lakini watakaobaki hawataondolewa kutoka mjini.
Da samler jeg alle Folkene til Angreb paa Jerusalem; Byen indtages, Husene plyndres, Kvinderne skændes, og Halvdelen af Byens Indbyggere vandrer i Landflygtighed; men Resten af Folket skal ikke udryddes af Byen.
3 Kisha Bwana atatoka na kupigana dhidi ya watu wa yale mataifa, kama apiganavyo siku ya vita.
Og HERREN drager ud og strider mod disse Folk, som han fordum stred paa Kampens Dag.
4 Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, mashariki mwa Yerusalemu, nao Mlima wa Mizeituni utagawanyika mara mbili kuanzia mashariki hadi magharibi, ukifanya bonde kubwa, nusu ya mlima ukisogea kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
Paa hin Dag staar hans Fødder paa Oliebjerget østen for Jerusalem, og Oliebjerget skal revne midt over fra Øst til Vest og danne en vældig Dal, idet Bjergets ene Halvdel viger mod Nord, den anden mod Syd.
5 Nanyi mtakimbia kupitia katika bonde hilo la mlima wangu kwa kuwa litaenea hadi Aseli. Mtakimbia kama mlivyokimbia tetemeko la ardhi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda. Kisha Bwana Mungu wangu atakuja na watakatifu wote pamoja naye.
I skal flygte til mine Bjerges Dal, thi Bjergdalen naar til Azal. I skal fly, som I flyede for Jordskælvet i Kong Uzzija af Judas Dage. Og HERREN min Gud kommer og alle de Hellige med ham.
6 Siku hiyo hakutakuwepo nuru, baridi wala theluji.
Paa hin Dag skal der ikke være Hede eller Kulde og Frost.
7 Itakuwa siku ya kipekee, isiyo na mchana wala usiku, siku ijulikanayo na Bwana. Jioni inapofika nuru itakuwepo.
Det skal være een eneste Dag — HERREN kender den — ikke Dag og Nat; det skal være lyst ved Aftentide.
8 Siku hiyo, maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu, nusu kwenda kwenye bahari ya mashariki, na nusu kwenda kwenye bahari ya magharibi wakati wa kiangazi na wakati wa masika.
Paa hin Dag skal rindende Vand vælde frem fra Jerusalem; det halve løber ud i Havet mod Øst, det halve i Havet mod Vest, og det baade Sommer og Vinter.
9 Bwana atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo atakuwepo Bwana mmoja na jina lake litakuwa jina pekee.
Og HERREN skal være Konge over hele Jorden. Paa hin Dag skal HERREN være een og hans Navn eet.
10 Nchi yote kuanzia Geba, kaskazini mwa Yuda, hadi Rimoni, kusini mwa Yerusalemu, itakuwa kama Araba. Lakini Yerusalemu utainuliwa juu na kubaki mahali pake, toka Lango la Benyamini hadi mahali pa Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni na kutoka Mnara wa Hananeli hadi kwenye mashinikizo ya divai ya mfalme.
Og hele Landet bliver en Slette fra Geba til Rimmon i Sydlandet; men Jerusalem skal ligge højt paa sit gamle Sted. Fra Benjaminsporten til den gamle Ports Sted, til Hjørneporten, og fra Hanan'eltaarnet til de kongelige Vinperser skal det være beboet.
11 Utakaliwa na watu, kamwe hautaharibiwa tena, Yerusalemu utakaa salama.
Der skal ikke mere lægges Band derpaa, og Jerusalem skal ligge trygt.
12 Hii ndiyo tauni ambayo Bwana atapiga nayo mataifa yote ambayo yalipigana dhidi ya Yerusalemu: Nyama ya miili yao itaoza wangali wamesimama kwa miguu yao, macho yao yataoza kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza vinywani mwao.
Men dette skal være den Plage, HERREN lader ramme alle de Folkeslag, som drager i Leding mod Jerusalem: han lader Kødet raadne paa dem i levende Live, Øjnene raadner i deres Øjenhuler og Tungen i deres Mund.
13 Katika siku hiyo Bwana atawatia wanaume hofu kuu. Kila mwanaume atakamata mkono wa mwenzake nao watashambuliana.
Paa hin Dag skal en vældig HERRENS Rædsel opstaa iblandt dem, saa de griber fat i og løfter Haand mod hverandre.
14 Yuda pia atapigana katika Yerusalemu. Utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka Yerusalemu utakusanywa, wingi wa dhahabu, fedha na nguo.
Ogsaa Juda skal stride i Jerusalem. Og alle Folkenes Rigdom skal samles trindt om fra, Guld, Sølv og Klæder i saare store Maader.
15 Tauni ya aina iyo hiyo itapiga farasi na nyumbu, ngamia na punda, nao wanyama wote walioko kwenye kambi za adui.
Og samme Plage skal ramme Heste, Muldyr, Kameler, Æsler og alt Kvæg i Lejrene der.
16 Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
Men alle de, der bliver tilbage af alle Folkene, som kommer imod Jerusalem, skal Aar efter Aar drage derop for at tilbede Kongen, Hærskarers HERRE, og fejre Løvhyttefest.
17 Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao.
Og dersom nogen af Jordens Slægter ikke drager op til Jerusalem for at tilbede Kongen, Hærskarers HERRE, skal der ikke falde Regn hos dem.
18 Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. Bwana ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
Og dersom Ægyptens Slægt ikke drager derop og kommer derhen, saa skal de rammes af den Plage, HERREN lader ramme Folkene.
19 Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
Det er Straffen over Ægypterne og alle de Folk, som ikke drager op for at fejre Løvhyttefest.
20 Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: Takatifu kwa Bwana, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya Bwana vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu.
Paa hin Dag skal der staa paa Hestenes Bjælder »Helliget HERREN«. Og Gryderne i HERRENS Hus skal være som Offerskaalene for Alteret;
21 Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote.
hver Gryde i Jerusalem og Juda skal være helliget Hærskarers HERRE, saa alle de ofrende kan komme og tage af dem og koge deri. Og paa hin Dag skal der ikke mere være nogen Kana'anæer i Hærskarers HERRES Hus.

< Zekaria 14 >