< Zekaria 13 >
1 “Katika siku hiyo, chemchemi itafunguliwa kwa nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu, kuwatakasa dhambi na unajisi.
En ce jour tout lieu sera ouvert à la maison de David et aux habitants de Jérusalem, pour le départ et la séparation.
2 “Katika siku hiyo, nitayakatilia mbali majina ya sanamu kutoka nchi, nayo hayatakumbukwa tena,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Nitaondoa manabii wao pamoja na roho ya uchafu katika nchi.
Et ce jour-là voici ce qui arrivera, dit le Seigneur Dieu des armées: J'effacerai les noms des idoles sur la terre, et il n'y aura plus de ces noms aucun souvenir; et J'exterminerai de la terre les faux prophètes et l'esprit immonde.
3 Ikiwa yupo yeyote atakayeendelea kutabiri, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, ‘Ni lazima ufe, kwa sababu umesema uongo kwa jina la Bwana.’ Atakapotabiri, wazazi wake mwenyewe watampasua tumbo.
Et voici ce qui arrivera: si un homme prophétise encore, son père et sa mère qui l'ont engendré lui diront: Tu mourras, parce que tu as dit des mensonges au Nom du Seigneur. Et son père et sa mère qui l'ont engendré l'empêcheront de prophétiser.
4 “Katika siku hiyo, kila nabii ataaibika kwa maono ya unabii wake. Hatavaa vazi la kinabii la nywele ili apate kudanganya watu.
Et ce jour-là voici ce qui arrivera: les prophètes menteurs seront confondus, chacun par la vision même pour laquelle il aura prophétisé, et ils se ceindront de cilice de crin, parce qu'ils auront menti.
5 Atasema, ‘Mimi sio nabii. Mimi ni mkulima; ardhi imekuwa kazi yangu tangu ujana wangu.’
Et chacun d'eux dira: Je ne suis point prophète; je suis un homme travaillant la terre, et c'est un homme qui m'a donné le jour, et m'a ainsi élevé depuis ma jeunesse.
6 Ikiwa mtu atamuuliza, ‘Majeraha haya yaliyo mwilini mwako ni ya nini?’ Atajibu, ‘Ni majeraha niliyoyapata katika nyumba ya rafiki zangu.’
Et Je lui dirai: Qu'est-ce que ces plaies que Tu as au milieu des mains? Et Il répondra: Ce sont les plaies que J'ai reçues dans une maison bien-aimée.
7 “Amka, ee upanga, dhidi ya mchungaji wangu, dhidi ya mtu aliye karibu nami!” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika, nami nitageuza mkono wangu dhidi ya walio wadogo,
Glaive, lève-toi contre Mes pasteurs et contre l'homme qui habite Ma ville, dit le Seigneur tout-puissant; frappez le berger, enlevez les brebis, et J'étendrai Ma main sur les petits.
8 katika nchi yote,” asema Bwana, “theluthi mbili watapigwa na kuangamia; hata hivyo theluthi moja watabaki ndani yake.
Et voici ce qui arrivera sur toute la terre, dit le Seigneur: J'en exterminerai deux parts, elles périront; et la troisième part sera épargnée.
9 Hii theluthi moja nitaileta katika moto; nitawasafisha kama fedha isafishwavyo na kuwajaribu kama dhahabu. Wataliitia Jina langu nami nitawajibu; nitasema, ‘Hawa ni watu wangu,’ nao watasema, ‘Bwana ni Mungu wetu.’”
Et Je ferai passer la troisième part dans la flamme, et Je la purifierai au feu, comme on purifie l'argent, et Je l'éprouverai comme on éprouve l'or. Elle invoquera Mon Nom, et Je l'exaucerai; et Je dirai: Voici Mon peuple; et elle dira: Le Seigneur est mon Dieu.