< Zekaria 13 >
1 “Katika siku hiyo, chemchemi itafunguliwa kwa nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu, kuwatakasa dhambi na unajisi.
En ce jour-là, il y aura une source ouverte à la maison de David et aux habitants de Jérusalem pour laver le péché et la souillure.
2 “Katika siku hiyo, nitayakatilia mbali majina ya sanamu kutoka nchi, nayo hayatakumbukwa tena,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Nitaondoa manabii wao pamoja na roho ya uchafu katika nchi.
Et il arrivera en ce jour-là, – oracle de Yahweh des armées: J’abolirai du pays les noms des idoles, et on n’en fera plus mention; et j’ôterai aussi du pays les prophètes et l’esprit d’impureté.
3 Ikiwa yupo yeyote atakayeendelea kutabiri, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, ‘Ni lazima ufe, kwa sababu umesema uongo kwa jina la Bwana.’ Atakapotabiri, wazazi wake mwenyewe watampasua tumbo.
Et si quelqu’un prophétise encore, son père et sa mère, qui l’ont engendré, lui diront: « Tu ne vivras pas, car tu as dit des mensonges, au nom de Yahweh! « Et son père et sa mère, qui l’ont engendré, le transperceront pendant qu’il prophétisera.
4 “Katika siku hiyo, kila nabii ataaibika kwa maono ya unabii wake. Hatavaa vazi la kinabii la nywele ili apate kudanganya watu.
Et il arrivera en ce jour-là: Les prophètes auront honte, chacun de sa vision quand il prophétisera, et ils ne revêtiront plus le manteau de poil, en vue de mentir.
5 Atasema, ‘Mimi sio nabii. Mimi ni mkulima; ardhi imekuwa kazi yangu tangu ujana wangu.’
Tel dira: « Je ne suis pas prophète, moi; moi, je suis un homme qui cultive la terre, car un homme m’a acheté dès ma jeunesse. »
6 Ikiwa mtu atamuuliza, ‘Majeraha haya yaliyo mwilini mwako ni ya nini?’ Atajibu, ‘Ni majeraha niliyoyapata katika nyumba ya rafiki zangu.’
Et on lui dira: « Qu’est-ce que ces blessures à tes mains? « et il répondra: « J’ai reçu ces coups dans la maison de mes amis. »
7 “Amka, ee upanga, dhidi ya mchungaji wangu, dhidi ya mtu aliye karibu nami!” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika, nami nitageuza mkono wangu dhidi ya walio wadogo,
Epée, réveille-toi contre mon pasteur, contre l’homme qui est mon compagnon, – oracle de Yahweh des armées! Frappe le pasteur, et que le troupeau soit dispersé. Et je ramènerai ma main sur les petit.
8 katika nchi yote,” asema Bwana, “theluthi mbili watapigwa na kuangamia; hata hivyo theluthi moja watabaki ndani yake.
Et dans tout le pays, – oracle de Yahweh, – les deux tiers seront exterminés, périront, et l’ autre tiers y sera laissé.
9 Hii theluthi moja nitaileta katika moto; nitawasafisha kama fedha isafishwavyo na kuwajaribu kama dhahabu. Wataliitia Jina langu nami nitawajibu; nitasema, ‘Hawa ni watu wangu,’ nao watasema, ‘Bwana ni Mungu wetu.’”