< Zekaria 13 >

1 “Katika siku hiyo, chemchemi itafunguliwa kwa nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu, kuwatakasa dhambi na unajisi.
In that day there shall be a fountain opened To the house of David, and to the inhabitants of Jerusalem, For sin and for uncleanness.
2 “Katika siku hiyo, nitayakatilia mbali majina ya sanamu kutoka nchi, nayo hayatakumbukwa tena,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Nitaondoa manabii wao pamoja na roho ya uchafu katika nchi.
And it shall come to pass in that day, Saith Jehovah of hosts, That I will cut off the names of the idols out of the land, And they shall no more be remembered; And the prophets also, and the impure spirit, Will I cause to pass out of the land.
3 Ikiwa yupo yeyote atakayeendelea kutabiri, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, ‘Ni lazima ufe, kwa sababu umesema uongo kwa jina la Bwana.’ Atakapotabiri, wazazi wake mwenyewe watampasua tumbo.
And it shall come to pass, when any one shall yet prophesy, That his father and mother shall say to him, Even they that begat him, “Thou shalt not live; For thou hast spoken falsehood in the name of Jehovah.” And his father and mother that begat him shall pierce him through when he prophesieth.
4 “Katika siku hiyo, kila nabii ataaibika kwa maono ya unabii wake. Hatavaa vazi la kinabii la nywele ili apate kudanganya watu.
And it shall come to pass in that day, that the prophet shall be ashamed Every one of his vision when he prophesieth; Neither shall they wear a garment of hair, to deceive.
5 Atasema, ‘Mimi sio nabii. Mimi ni mkulima; ardhi imekuwa kazi yangu tangu ujana wangu.’
But each shall say, “I am no prophet; I am a man that tilleth the ground; For a man hath purchased me from my youth.”
6 Ikiwa mtu atamuuliza, ‘Majeraha haya yaliyo mwilini mwako ni ya nini?’ Atajibu, ‘Ni majeraha niliyoyapata katika nyumba ya rafiki zangu.’
And when one shall say to him, “What are these wounds in thy hands?” He shall answer, “Those with which I was wounded in the house of my friends.”
7 “Amka, ee upanga, dhidi ya mchungaji wangu, dhidi ya mtu aliye karibu nami!” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika, nami nitageuza mkono wangu dhidi ya walio wadogo,
Awake, O sword, against my shepherd, Even against the man who is my fellow, saith Jehovah of hosts! Smite the shepherd, and let the sheep be scattered! I will also turn my hand against the lambs.
8 katika nchi yote,” asema Bwana, “theluthi mbili watapigwa na kuangamia; hata hivyo theluthi moja watabaki ndani yake.
And it shall come to pass in all the land, saith Jehovah, That two parts therein shall be cut off and die; But the third part shall be left therein.
9 Hii theluthi moja nitaileta katika moto; nitawasafisha kama fedha isafishwavyo na kuwajaribu kama dhahabu. Wataliitia Jina langu nami nitawajibu; nitasema, ‘Hawa ni watu wangu,’ nao watasema, ‘Bwana ni Mungu wetu.’”
And I will bring the third part through the fire, And will refine them, as silver is refined, And will try them, as gold is tried; They shall call upon me, and I will hear them; I will say, “It is my people.” And they shall say, “Jehovah is our God.”

< Zekaria 13 >