< Zekaria 13 >

1 “Katika siku hiyo, chemchemi itafunguliwa kwa nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu, kuwatakasa dhambi na unajisi.
In that day there shall be a fountain open to the house of David, and to the inhabitants of Jerusalem: for the washing of the sinner, and of the unclean woman.
2 “Katika siku hiyo, nitayakatilia mbali majina ya sanamu kutoka nchi, nayo hayatakumbukwa tena,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Nitaondoa manabii wao pamoja na roho ya uchafu katika nchi.
And it shall come to pass in that day, saith the Lord of hosts, that I will destroy the names of idols out of the earth, and they shall be remembered no more: and I will take away the false prophets, and the unclean spirit out of the earth.
3 Ikiwa yupo yeyote atakayeendelea kutabiri, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, ‘Ni lazima ufe, kwa sababu umesema uongo kwa jina la Bwana.’ Atakapotabiri, wazazi wake mwenyewe watampasua tumbo.
And it shall come to pass, that when any man shall prophesy any more, his father and his mother that brought him into the world, shall say to him: Thou shalt not live: because thou best spoken a lie in the name of the Lord. And his father, and his mother, his parents, shall thrust him through, when he shall prophesy.
4 “Katika siku hiyo, kila nabii ataaibika kwa maono ya unabii wake. Hatavaa vazi la kinabii la nywele ili apate kudanganya watu.
And it shall come to pass in that day, that the prophets shall be confounded, every one by his own vision, when he shall prophesy, neither shall they be clad with a garment of sackcloth, to deceive:
5 Atasema, ‘Mimi sio nabii. Mimi ni mkulima; ardhi imekuwa kazi yangu tangu ujana wangu.’
But he shall say: I am no prophet, I am a husbandman: for Adam is my example from my youth.
6 Ikiwa mtu atamuuliza, ‘Majeraha haya yaliyo mwilini mwako ni ya nini?’ Atajibu, ‘Ni majeraha niliyoyapata katika nyumba ya rafiki zangu.’
And they shall say to him: What are these wounds in the midst of thy hands? And he shall say: With these I was wounded in the house of them that loved me.
7 “Amka, ee upanga, dhidi ya mchungaji wangu, dhidi ya mtu aliye karibu nami!” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika, nami nitageuza mkono wangu dhidi ya walio wadogo,
Awake, O sword, against my shepherd, and against the man that cleaveth to me, saith the Lord of hosts: strike the shepherd, and the sheep shall be scattered: and I will turn my hand to the little ones.
8 katika nchi yote,” asema Bwana, “theluthi mbili watapigwa na kuangamia; hata hivyo theluthi moja watabaki ndani yake.
And there shall be in all the earth, saith the Lord, two parts in it shall be scattered, and shall perish: but the third part shall be left therein.
9 Hii theluthi moja nitaileta katika moto; nitawasafisha kama fedha isafishwavyo na kuwajaribu kama dhahabu. Wataliitia Jina langu nami nitawajibu; nitasema, ‘Hawa ni watu wangu,’ nao watasema, ‘Bwana ni Mungu wetu.’”
And I will bring the third part through the fire, and will refine them as silver is refined: and I will try them as gold is tried. They shall call on my name, and I will hear them. I will say: Thou art my people: and they shall say: The Lord is my God.

< Zekaria 13 >