< Zekaria 12 >
1 Hili ni neno la Bwana kuhusu Israeli. Bwana, yeye azitandaye mbingu, awekaye misingi ya dunia na aiumbaye roho ya mwanadamu ndani yake, asema:
Révélation de la parole de Yahvé concernant Israël: Yahvé, qui étend les cieux et pose les fondements de la terre, et qui forme en lui l'esprit de l'homme, dit:
2 “Nitakwenda kufanya Yerusalemu kuwa kikombe cha kuyumbisha mataifa yote yanayoizunguka. Yuda utazingirwa kwa vita na Yerusalemu pia.
« Voici, je ferai de Jérusalem une coupe de roulis pour tous les peuples d'alentour, et il en sera de même pour Juda lors du siège de Jérusalem.
3 Katika siku hiyo, wakati mataifa yote ya dunia yatakapokusanyika dhidi yake, nitaufanya Yerusalemu kuwa jabali lisilosogezwa kwa mataifa yote. Wote watakaojaribu kulisogeza watajiumiza wenyewe.
Il arrivera en ce jour-là que je ferai de Jérusalem une pierre pesante pour tous les peuples. Tous ceux qui s'en chargeront seront gravement blessés, et toutes les nations de la terre s'assembleront contre elle.
4 Katika siku hiyo nitampiga kila farasi kwa hofu ya ghafula, naye ampandaye nitampiga kwa uwazimu,” asema Bwana. “Nitalielekeza jicho langu la ulinzi juu ya nyumba ya Yuda, nami nitawapofusha farasi wote wa mataifa.
En ce jour-là, dit Yahvé, je frapperai de terreur tout cheval et de folie son cavalier. J'ouvrirai mes yeux sur la maison de Juda, et je frapperai d'aveuglement tous les chevaux des peuples.
5 Kisha viongozi wa Yuda watasema mioyoni mwao, ‘Watu wa Yerusalemu wana nguvu kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote ni Mungu wao.’
Les chefs de Juda diront en leur cœur: « Les habitants de Jérusalem sont ma force dans l'Éternel des armées, leur Dieu ».
6 “Katika siku hiyo nitawafanya viongozi wa Yuda kuwa kama kigae cha moto ndani ya lundo la kuni, kama mwenge uwakao kati ya miganda. Watateketeza kulia na kushoto mataifa yote yanayowazunguka, lakini Yerusalemu utabaki salama mahali pake.
En ce jour-là, je ferai des chefs de Juda comme une poêle de feu au milieu du bois, et comme une torche enflammée au milieu des gerbes. Ils dévoreront tous les peuples d'alentour, à droite et à gauche, et Jérusalem habitera encore dans son lieu propre, à Jérusalem.
7 “Bwana atayaokoa makao ya Yuda kwanza, ili heshima ya nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu isiwe kubwa zaidi kuliko ile ya Yuda.
Yahvé sauvera aussi d'abord les tentes de Juda, afin que la gloire de la maison de David et la gloire des habitants de Jérusalem ne soient pas élevées au-dessus de Juda.
8 Katika siku hiyo, Bwana atawakinga wale waishio Yerusalemu, ili kwamba aliye dhaifu kupita wote miongoni mwao awe kama Daudi, nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama Malaika wa Bwana akiwatangulia.
En ce jour-là, Yahvé défendra les habitants de Jérusalem. Celui d'entre eux qui sera faible en ce jour-là sera comme David, et la maison de David sera comme Dieu, comme l'ange de Yahvé devant eux.
9 Katika siku hiyo nitatoka kuangamiza mataifa yote yatakayoshambulia Yerusalemu.
En ce jour-là, je chercherai à détruire toutes les nations qui viendront contre Jérusalem.
10 “Nami nitamiminia nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu roho ya neema na maombi. Watanitazama mimi, yule waliyemchoma. Nao watamwombolezea kama mtu anayemwombolezea mwanawe wa pekee na kusikitika kwa uchungu kama anayemsikitikia mzaliwa wake wa kwanza wa kiume.
Je répandrai sur la maison de David et sur les habitants de Jérusalem un esprit de grâce et de supplication. Ils regarderont vers moi, qu'ils ont percé, et ils le pleureront comme on pleure son fils unique, et ils en éprouveront une amère tristesse comme on éprouve une tristesse pour son premier-né.
11 Katika siku hiyo kilio kitakuwa kikubwa Yerusalemu, kama kilio cha Hadad-Rimoni katika tambarare ya Megido.
En ce jour-là, il y aura un grand deuil à Jérusalem, comme le deuil d'Hadadrimmon dans la vallée de Megiddo.
12 Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yake, nao wake zao peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi na wake zao, ukoo wa nyumba ya Nathani na wake zao,
Le pays sera dans le deuil, toutes les familles à part: la famille de la maison de David et ses femmes à part; la famille de la maison de Nathan et ses femmes à part;
13 ukoo wa nyumba ya Lawi na wake zao, ukoo wa Shimei na wake zao,
la famille de la maison de Lévi et ses femmes à part; la famille des Shiméites et ses femmes à part;
14 na koo zote zilizobaki na wake zao.
toutes les familles qui resteront, toutes les familles à part et leurs femmes à part.