< Zekaria 12 >
1 Hili ni neno la Bwana kuhusu Israeli. Bwana, yeye azitandaye mbingu, awekaye misingi ya dunia na aiumbaye roho ya mwanadamu ndani yake, asema:
[the] oracle of [the] word of Yahweh on Israel [the] utterance of Yahweh [who] stretched out heaven and [who] founded earth and [who] formed [the] spirit of a human in inner being his.
2 “Nitakwenda kufanya Yerusalemu kuwa kikombe cha kuyumbisha mataifa yote yanayoizunguka. Yuda utazingirwa kwa vita na Yerusalemu pia.
Here! I [am] about to make Jerusalem a basin of reeling for all the peoples all around and also on Judah it will be in the siege on Jerusalem.
3 Katika siku hiyo, wakati mataifa yote ya dunia yatakapokusanyika dhidi yake, nitaufanya Yerusalemu kuwa jabali lisilosogezwa kwa mataifa yote. Wote watakaojaribu kulisogeza watajiumiza wenyewe.
And it will be on the day that I will make Jerusalem a stone of burden for all the peoples all [those who] carry it severely they will injure themselves and they will gather on it all [the] nations of the earth.
4 Katika siku hiyo nitampiga kila farasi kwa hofu ya ghafula, naye ampandaye nitampiga kwa uwazimu,” asema Bwana. “Nitalielekeza jicho langu la ulinzi juu ya nyumba ya Yuda, nami nitawapofusha farasi wote wa mataifa.
On the day that [the] utterance of Yahweh I will strike every horse with bewilderment and rider its with madness and over [the] house of Judah I will open eyes my and every horse of the peoples I will strike with blindness.
5 Kisha viongozi wa Yuda watasema mioyoni mwao, ‘Watu wa Yerusalemu wana nguvu kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote ni Mungu wao.’
And they will say [the] chiefs of Judah in heart their [are] strength of me [the] inhabitants of Jerusalem by Yahweh of hosts God their.
6 “Katika siku hiyo nitawafanya viongozi wa Yuda kuwa kama kigae cha moto ndani ya lundo la kuni, kama mwenge uwakao kati ya miganda. Watateketeza kulia na kushoto mataifa yote yanayowazunguka, lakini Yerusalemu utabaki salama mahali pake.
On the day that I will make [the] chiefs of Judah like a pot of fire among wood and like a torch of fire among cut grain and they will consume on [the] right [side] and on [the] left [side] all the peoples all around and it will remain Jerusalem again in place its in Jerusalem.
7 “Bwana atayaokoa makao ya Yuda kwanza, ili heshima ya nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu isiwe kubwa zaidi kuliko ile ya Yuda.
And he will save Yahweh [the] tents of Judah at the first so that not it will be great [the] splendor of [the] house of David and [the] splendor of [the] inhabitant[s] of Jerusalem above Judah.
8 Katika siku hiyo, Bwana atawakinga wale waishio Yerusalemu, ili kwamba aliye dhaifu kupita wote miongoni mwao awe kama Daudi, nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama Malaika wa Bwana akiwatangulia.
On the day that he will defend Yahweh for [the] inhabitant[s] of Jerusalem and he will be the [one who] stumbles among them on the day that like David and [the] house of David [will be] like God like [the] angel of Yahweh before them.
9 Katika siku hiyo nitatoka kuangamiza mataifa yote yatakayoshambulia Yerusalemu.
And it will be on the day that I will seek to destroy all the nations that are coming on Jerusalem.
10 “Nami nitamiminia nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu roho ya neema na maombi. Watanitazama mimi, yule waliyemchoma. Nao watamwombolezea kama mtu anayemwombolezea mwanawe wa pekee na kusikitika kwa uchungu kama anayemsikitikia mzaliwa wake wa kwanza wa kiume.
And I will pour out on [the] house of David and on - [the] inhabitant[s] of Jerusalem a spirit of favor and supplications and they will look to me [the one] whom they have pierced through and they will mourn on him like mourning on only [son] and they will show bitterness on him as shows bitterness on firstborn.
11 Katika siku hiyo kilio kitakuwa kikubwa Yerusalemu, kama kilio cha Hadad-Rimoni katika tambarare ya Megido.
On the day that it will be great the mourning in Jerusalem like [the] mourning of Hadad-Rimmon in [the] plain of Megiddo.
12 Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yake, nao wake zao peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi na wake zao, ukoo wa nyumba ya Nathani na wake zao,
And it will mourn the land clans clans alone [the] clan of [the] house of David alone and wives their alone [the] clan of [the] house of Nathan alone and wives their alone.
13 ukoo wa nyumba ya Lawi na wake zao, ukoo wa Shimei na wake zao,
[the] clan of [the] house of Levi alone and wives their alone [the] clan of the Shimeite[s] alone and wives their alone.
14 na koo zote zilizobaki na wake zao.
All the clans which remain clans clans alone and wives their alone.