< Zekaria 12 >
1 Hili ni neno la Bwana kuhusu Israeli. Bwana, yeye azitandaye mbingu, awekaye misingi ya dunia na aiumbaye roho ya mwanadamu ndani yake, asema:
The prophecy of the word of Jehovah concerning Israel. Thus saith Jehovah, who stretched out the heavens, And laid the foundation of the earth, And formed the spirit of man within him:
2 “Nitakwenda kufanya Yerusalemu kuwa kikombe cha kuyumbisha mataifa yote yanayoizunguka. Yuda utazingirwa kwa vita na Yerusalemu pia.
Behold, I make Jerusalem a cup of giddiness to all the nations round about, And for Judah also shall it be In the siege against Jerusalem.
3 Katika siku hiyo, wakati mataifa yote ya dunia yatakapokusanyika dhidi yake, nitaufanya Yerusalemu kuwa jabali lisilosogezwa kwa mataifa yote. Wote watakaojaribu kulisogeza watajiumiza wenyewe.
And in that day will I make Jerusalem A burdensome stone for all nations; All that lift it up shall tear themselves, And all the nations of the earth shall gather themselves together against it.
4 Katika siku hiyo nitampiga kila farasi kwa hofu ya ghafula, naye ampandaye nitampiga kwa uwazimu,” asema Bwana. “Nitalielekeza jicho langu la ulinzi juu ya nyumba ya Yuda, nami nitawapofusha farasi wote wa mataifa.
In that day, saith Jehovah, I will smite every horse with amazement, And his rider with madness; I will open mine eyes upon the house of Judah, And every horse of the nations will I smite with blindness.
5 Kisha viongozi wa Yuda watasema mioyoni mwao, ‘Watu wa Yerusalemu wana nguvu kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote ni Mungu wao.’
Then shall the leaders of Judah say in their heart, “Strong are the inhabitants of Jerusalem, Through Jehovah of hosts, their God.”
6 “Katika siku hiyo nitawafanya viongozi wa Yuda kuwa kama kigae cha moto ndani ya lundo la kuni, kama mwenge uwakao kati ya miganda. Watateketeza kulia na kushoto mataifa yote yanayowazunguka, lakini Yerusalemu utabaki salama mahali pake.
In that day will I make the leaders of Judah Like a fire-pan among wood, And like a torch of fire in a sheaf, And they shall devour, on the right hand and on the left, All the nations round about. And Jerusalem shall again dwell in her own place at Jerusalem.
7 “Bwana atayaokoa makao ya Yuda kwanza, ili heshima ya nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu isiwe kubwa zaidi kuliko ile ya Yuda.
Jehovah will also save the tents of Judah first, That the glory of the house of David, And the glory of the inhabitants of Jerusalem, May not magnify itself against Judah.
8 Katika siku hiyo, Bwana atawakinga wale waishio Yerusalemu, ili kwamba aliye dhaifu kupita wote miongoni mwao awe kama Daudi, nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama Malaika wa Bwana akiwatangulia.
In that day shall Jehovah defend the inhabitants of Jerusalem, And he that is feeble among them in that day shall be like David, And the house of David shall be as God, As the angel of Jehovah before them.
9 Katika siku hiyo nitatoka kuangamiza mataifa yote yatakayoshambulia Yerusalemu.
And it shall come to pass in that day That I will seek to destroy all the nations Which come against Jerusalem.
10 “Nami nitamiminia nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu roho ya neema na maombi. Watanitazama mimi, yule waliyemchoma. Nao watamwombolezea kama mtu anayemwombolezea mwanawe wa pekee na kusikitika kwa uchungu kama anayemsikitikia mzaliwa wake wa kwanza wa kiume.
Then will I pour upon the house of David, And upon the inhabitants of Jerusalem, A spirit of supplication, and of prayer; And they shall look to me whom they pierced, And they shall mourn for him, as one mourneth for his only son, And shall be in bitterness for him, as one that is in bitterness for his first-born.
11 Katika siku hiyo kilio kitakuwa kikubwa Yerusalemu, kama kilio cha Hadad-Rimoni katika tambarare ya Megido.
In that day the mourning shall be great in Jerusalem, As the mourning of Hadadrimmon in the valley of Megiddo.
12 Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yake, nao wake zao peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi na wake zao, ukoo wa nyumba ya Nathani na wake zao,
And the land shall mourn, every family apart; The family of the house of David apart, and their wives apart; The family of the house of Nathan apart, and their wives apart;
13 ukoo wa nyumba ya Lawi na wake zao, ukoo wa Shimei na wake zao,
The family of the house of Levi apart, and their wives apart; The family of the house of Shimei apart, and their wives apart;
14 na koo zote zilizobaki na wake zao.
All the families that remain, Every family apart, and their wives apart.