< Zekaria 10 >
1 Mwombeni Bwana mvua wakati wa vuli; ndiye Bwana atengenezaye mawingu ya tufani. Huwapa watu manyunyu ya mvua, pia mimea ya shambani kwa ajili ya kila mtu.
Pide al Señor lluvia, en el tiempo de las lluvias de primavera, al Señor que hace relámpagos; y él les dará lluvias en abundancia hierba a cada hombre que esté en el campo.
2 Sanamu huzungumza udanganyifu, waaguzi huona maono ya uongo; husimulia ndoto ambazo si za kweli, wanatoa faraja batili. Kwa hiyo watu wanatangatanga kama kondoo walioonewa kwa kukosa mchungaji.
Porque las imágenes han dicho lo que no es verdad, y es mentira lo que ven los adivinos; han dado cuenta de sueños falsos, su consuelo no tiene propósito; por lo que salen del camino como ovejas, están preocupados porque no tienen pastor.
3 “Hasira yangu inawaka dhidi ya wachungaji, nami nitawaadhibu viongozi; kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote atalichunga kundi lake, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi mwenye kiburi akiwa vitani.
Mi ira arde contra los pastores del rebaño, y enviaré castigo a los machos cabríos; porque el Señor de los ejércitos ha visitado a su rebaño, el pueblo de Judá, y los hará como el caballo de esplendor en la lucha.
4 Kutoka Yuda litatokea Jiwe la pembeni, kutoka kwake vitatoka vigingi vya hema, kutoka kwake utatoka upinde wa vita, kutoka kwake atatoka kila mtawala.
De él saldrá la piedra angular, de él la estaca de la tienda, de él el arco de guerra, de él saldrá todo gobernante;
5 Kwa pamoja watakuwa kama mashujaa wanaokanyaga barabara za matope wakati wa vita. Kwa sababu Bwana yu pamoja nao, watapigana na kuwashinda wapanda farasi.
Juntos serán como hombres de guerra, aplastando a sus enemigos en la tierra de las calles en la lucha; pelearán porque el Señor está con ellos, y los jinetes serán avergonzados.
6 “Nitaiimarisha nyumba ya Yuda na kuiokoa nyumba ya Yosefu. Nitawarejesha kwa sababu nina huruma juu yao. Watakuwa kama watu ambao sijawahi kuwakataa kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wao, nami nitawajibu.
Y haré fuertes a los hijos de Judá, y seré el salvador de los hijos de José, y los haré volver de nuevo, porque he tenido misericordia de ellos; serán como si yo nunca los hubiera rechazado; porque yo soy el Señor su Dios y les daré una respuesta.
7 Waefraimu watakuwa kama mashujaa, mioyo yao itafurahi kana kwamba ni kwa divai. Watoto wao wataona na kufurahi, mioyo yao itashangilia katika Bwana.
Y Efraín será como un hombre de guerra, y su corazón se alegrará como con el vino; y sus hijos lo verán con alegría; su corazón se alegrará en el Señor.
8 Nitawaashiria na kuwakusanya ndani. Hakika nitawakomboa, nao watakuwa wengi kama walivyokuwa mwanzoni.
Y les silbaré para reunirlos; porque los he redimido: y se incrementarán como fueron incrementados antes.
9 Ijapokuwa niliwatawanya miongoni mwa mataifa, hata hivyo wakiwa katika nchi za mbali watanikumbuka mimi. Wao na watoto wao watanusurika katika hatari nao watarudi.
Aunque los sembrare entre los pueblos, me recordarán en países lejanos, y cuidarán a sus hijos y volverán.
10 Nitawarudisha kutoka Misri na kuwakusanya toka Ashuru. Nitawaleta katika nchi ya Gileadi na Lebanoni, na hapo hapatakuwa na nafasi ya kuwatosha.
Y haré que regresen de la tierra de Egipto, y los juntaré de Asiria; y los llevaré a la tierra de Galaad y al Líbano, serán tantos y no será lo suficientemente ancho para ellos.
11 Watapita katika bahari ya mateso; bahari iliyochafuka itatulizwa na vilindi vyote vya Mto Naili vitakauka. Kiburi cha Ashuru kitashushwa, nayo fimbo ya utawala ya Misri itatoweka.
Y atravesarán el mar de Egipto, y todas las aguas profundas del Nilo se secarán; y el orgullo de Asiria será abatido, y el poder de Egipto será quitado.
12 Nitawaimarisha katika Bwana, na katika jina lake watatembea,” asema Bwana.
Y su fortaleza estará en el Señor; y caminarán en su nombre, dice el Señor.