< Zekaria 10 >

1 Mwombeni Bwana mvua wakati wa vuli; ndiye Bwana atengenezaye mawingu ya tufani. Huwapa watu manyunyu ya mvua, pia mimea ya shambani kwa ajili ya kila mtu.
Demandez au Seigneur de la pluie selon la saison, le matin et le soir. Le Seigneur a créé des signes manifestes; Il donnera aux hommes les pluies d'hiver, et à chacun de l'herbe en son champ.
2 Sanamu huzungumza udanganyifu, waaguzi huona maono ya uongo; husimulia ndoto ambazo si za kweli, wanatoa faraja batili. Kwa hiyo watu wanatangatanga kama kondoo walioonewa kwa kukosa mchungaji.
Les faux prophètes ont fait des prédictions funestes; les devins ont rapporté des visions fausses et des songes trompeurs; ils ont donné de vaines consolations; à cause de cela, ils ont dépéri comme des brebis abandonnées; ils ont été affligés, parce qu'il n'y avait pas de remède.
3 “Hasira yangu inawaka dhidi ya wachungaji, nami nitawaadhibu viongozi; kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote atalichunga kundi lake, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi mwenye kiburi akiwa vitani.
Ma colère s'est enflammée contre les pasteurs, et Je visiterai les agneaux. Et le Seigneur Dieu tout-puissant visitera Son troupeau, la maison de Juda; et Il la formera comme son coursier, prêt aux combats.
4 Kutoka Yuda litatokea Jiwe la pembeni, kutoka kwake vitatoka vigingi vya hema, kutoka kwake utatoka upinde wa vita, kutoka kwake atatoka kila mtawala.
C'est de Lui que vient la visite; de Lui, l'ordre de bataille; de Lui, l'arc de la colère; et aussi tout exacteur sortira de Lui.
5 Kwa pamoja watakuwa kama mashujaa wanaokanyaga barabara za matope wakati wa vita. Kwa sababu Bwana yu pamoja nao, watapigana na kuwashinda wapanda farasi.
Et ils seront comme des guerriers, foulant aux pieds la boue des chemins dans la bataille; et ils en viendront aux mains, parce que le Seigneur sera avec eux; et les cavaliers seront confondus.
6 “Nitaiimarisha nyumba ya Yuda na kuiokoa nyumba ya Yosefu. Nitawarejesha kwa sababu nina huruma juu yao. Watakuwa kama watu ambao sijawahi kuwakataa kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wao, nami nitawajibu.
Et Je fortifierai la maison de Juda; et Je sauverai la maison de Joseph, et Je les rétablirai, parce que Je les aime; et ils seront comme si Je ne les avais pas répudiés; car Je suis le Seigneur leur Dieu, et Je les exaucerai.
7 Waefraimu watakuwa kama mashujaa, mioyo yao itafurahi kana kwamba ni kwa divai. Watoto wao wataona na kufurahi, mioyo yao itashangilia katika Bwana.
Et ils seront comme les guerriers d'Éphraïm, et leur cœur se réjouira, comme dans le vin; voilà ce que verront leurs enfants, et ils en seront charmés, et leur âme se réjouira dans le Seigneur.
8 Nitawaashiria na kuwakusanya ndani. Hakika nitawakomboa, nao watakuwa wengi kama walivyokuwa mwanzoni.
Je leur donnerai le signal et Je les rassemblerai; car Je les affranchirai et les multiplierai, comme lorsqu'ils étaient le plus nombreux.
9 Ijapokuwa niliwatawanya miongoni mwa mataifa, hata hivyo wakiwa katika nchi za mbali watanikumbuka mimi. Wao na watoto wao watanusurika katika hatari nao watarudi.
Et Je les disséminerai parmi les peuples, et les plus lointains se souviendront de Moi; ils élèveront leurs enfants, et ils reviendront de captivité.
10 Nitawarudisha kutoka Misri na kuwakusanya toka Ashuru. Nitawaleta katika nchi ya Gileadi na Lebanoni, na hapo hapatakuwa na nafasi ya kuwatosha.
Et Je les ramènerai de la terre d'Égypte; Je les accueillerai à leur retour de l'Assyrie, et Je les conduirai en Galaad et sur le Liban; et pas un seul d'entre eux ne sera laissé en oubli.
11 Watapita katika bahari ya mateso; bahari iliyochafuka itatulizwa na vilindi vyote vya Mto Naili vitakauka. Kiburi cha Ashuru kitashushwa, nayo fimbo ya utawala ya Misri itatoweka.
Et ils traverseront les détroits de la mer, et ils frapperont ses vagues, et le fond des fleuves sera à sec, et tout l'orgueil des Assyriens sera abattu, et le sceptre de l'Égypte sera brisé.
12 Nitawaimarisha katika Bwana, na katika jina lake watatembea,” asema Bwana.
Et Je les fortifierai dans le Seigneur leur Dieu; et ils se feront gloire de Son Nom, dit le Seigneur.

< Zekaria 10 >