< Zekaria 10 >

1 Mwombeni Bwana mvua wakati wa vuli; ndiye Bwana atengenezaye mawingu ya tufani. Huwapa watu manyunyu ya mvua, pia mimea ya shambani kwa ajili ya kila mtu.
Demandez à Yahweh de la pluie au printemps. C'est Yahweh qui fait les éclairs; il leur donnera une pluie abondante, à chacun de l'herbe dans son champ.
2 Sanamu huzungumza udanganyifu, waaguzi huona maono ya uongo; husimulia ndoto ambazo si za kweli, wanatoa faraja batili. Kwa hiyo watu wanatangatanga kama kondoo walioonewa kwa kukosa mchungaji.
Car les théraphim ont parlé futilité, et les devins ont eu des visions de mensonge; ils débitent de vains songes, et donnent de fausses consolations. C'est pourquoi ils sont partis comme un troupeau; ils ont été opprimés, faute de berger.
3 “Hasira yangu inawaka dhidi ya wachungaji, nami nitawaadhibu viongozi; kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote atalichunga kundi lake, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi mwenye kiburi akiwa vitani.
Ma colère s'est enflammée contre les bergers, et je châtierai les boucs! Car Yahweh des armées visite son troupeau, la maison de Juda, et il en fait son cheval d'honneur dans la bataille.
4 Kutoka Yuda litatokea Jiwe la pembeni, kutoka kwake vitatoka vigingi vya hema, kutoka kwake utatoka upinde wa vita, kutoka kwake atatoka kila mtawala.
De lui viendra la troupe, de lui le pieu, de lui l'arc de guerre; de lui sortiront tous les chefs ensemble.
5 Kwa pamoja watakuwa kama mashujaa wanaokanyaga barabara za matope wakati wa vita. Kwa sababu Bwana yu pamoja nao, watapigana na kuwashinda wapanda farasi.
Ils seront comme des héros, foulant la boue des chemins dans la bataille; ils combattront, car Yahweh sera avec eux, et ils couvriront de honte ceux qui sont montés sur des chevaux.
6 “Nitaiimarisha nyumba ya Yuda na kuiokoa nyumba ya Yosefu. Nitawarejesha kwa sababu nina huruma juu yao. Watakuwa kama watu ambao sijawahi kuwakataa kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wao, nami nitawajibu.
Je fortifierai la maison de Juda, et je sauverai la maison de Joseph; je les rétablirai, car j'ai compassion d'eux, et ils seront comme si je ne les avais pas rejetés. Car moi, je suis Yahweh, leur Dieu, et je les exaucerai.
7 Waefraimu watakuwa kama mashujaa, mioyo yao itafurahi kana kwamba ni kwa divai. Watoto wao wataona na kufurahi, mioyo yao itashangilia katika Bwana.
Ceux d'Ephraïm seront comme des héros, et leur cœur sera joyeux comme par le vin; leurs fils le verront et se réjouiront, et leur cœur tressaillira en Yahweh.
8 Nitawaashiria na kuwakusanya ndani. Hakika nitawakomboa, nao watakuwa wengi kama walivyokuwa mwanzoni.
Je sifflerai après eux, et je les rassemblerai, car je les ai rachetés, et ils se multiplieront comme ils s'étaient multipliés.
9 Ijapokuwa niliwatawanya miongoni mwa mataifa, hata hivyo wakiwa katika nchi za mbali watanikumbuka mimi. Wao na watoto wao watanusurika katika hatari nao watarudi.
Quand je les aurai répandus parmi les peuples, et qu'ils se souviendront de moi dans les pays lointains, ils vivront avec leurs enfants et ils reviendront.
10 Nitawarudisha kutoka Misri na kuwakusanya toka Ashuru. Nitawaleta katika nchi ya Gileadi na Lebanoni, na hapo hapatakuwa na nafasi ya kuwatosha.
Je les ramènerai du pays d'Egypte, et je les rassemblerai d'Assyrie, et je les ferai venir au pays de Galaad et au Liban, et il ne se trouvera pas assez d'espace pour eux.
11 Watapita katika bahari ya mateso; bahari iliyochafuka itatulizwa na vilindi vyote vya Mto Naili vitakauka. Kiburi cha Ashuru kitashushwa, nayo fimbo ya utawala ya Misri itatoweka.
Il passera par la mer, mer de détresse, il frappera les flots dans la mer, et toutes les profondeurs du fleuve seront mises à sec. L'orgueil de l'Assyrie sera abattu, et le sceptre de l'Egypte sera ôté.
12 Nitawaimarisha katika Bwana, na katika jina lake watatembea,” asema Bwana.
Je les fortifierai en Yahweh, et ils marcheront en son nom, — oracle de Yahweh.

< Zekaria 10 >