< Zekaria 10 >

1 Mwombeni Bwana mvua wakati wa vuli; ndiye Bwana atengenezaye mawingu ya tufani. Huwapa watu manyunyu ya mvua, pia mimea ya shambani kwa ajili ya kila mtu.
Aske you of the Lord raine in the time of the latter raine: so shall the Lord make white cloudes, and giue you showers of raine, and to euery one grasse in the field.
2 Sanamu huzungumza udanganyifu, waaguzi huona maono ya uongo; husimulia ndoto ambazo si za kweli, wanatoa faraja batili. Kwa hiyo watu wanatangatanga kama kondoo walioonewa kwa kukosa mchungaji.
Surely the idols haue spoken vanitie, and the southsayers haue seene a lye, and the dreamers haue tolde a vaine thing: they comfort in vaine: therefore they went away as sheepe: they were troubled, because there was no shepheard.
3 “Hasira yangu inawaka dhidi ya wachungaji, nami nitawaadhibu viongozi; kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote atalichunga kundi lake, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi mwenye kiburi akiwa vitani.
My wrath was kindled against the shepherdes, and I did visite the goates: but the Lord of hostes will visite his flocke the house of Iudah, and will make them as his beautifull horse in the battell.
4 Kutoka Yuda litatokea Jiwe la pembeni, kutoka kwake vitatoka vigingi vya hema, kutoka kwake utatoka upinde wa vita, kutoka kwake atatoka kila mtawala.
Out of him shall the corner come foorth: out of him the nayle, out of him ye bowe of battell, and out of him euery appointer of tribute also.
5 Kwa pamoja watakuwa kama mashujaa wanaokanyaga barabara za matope wakati wa vita. Kwa sababu Bwana yu pamoja nao, watapigana na kuwashinda wapanda farasi.
And they shalbe as the mightie men, which treade downe their enemies in the mire of the streetes in the battell, and they shall fight, because the Lord is with them, and the riders on horses shall be confounded.
6 “Nitaiimarisha nyumba ya Yuda na kuiokoa nyumba ya Yosefu. Nitawarejesha kwa sababu nina huruma juu yao. Watakuwa kama watu ambao sijawahi kuwakataa kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wao, nami nitawajibu.
And I will strengthen the house of Iudah, and I will preserue the house of Ioseph, and I wil bring them againe, for I pitie them: and they shall be as though I had not cast them off: for I am the Lord their God, and will heare them.
7 Waefraimu watakuwa kama mashujaa, mioyo yao itafurahi kana kwamba ni kwa divai. Watoto wao wataona na kufurahi, mioyo yao itashangilia katika Bwana.
And they of Ephraim shall be as a gyant, and their heart shall reioyce as thorowe wine: yea, their children shall see it, and be glad: and their heart shall reioyce in the Lord.
8 Nitawaashiria na kuwakusanya ndani. Hakika nitawakomboa, nao watakuwa wengi kama walivyokuwa mwanzoni.
I will hisse for them, and gather them: for I haue redeemed them: and they shall encrease, as they haue encreased.
9 Ijapokuwa niliwatawanya miongoni mwa mataifa, hata hivyo wakiwa katika nchi za mbali watanikumbuka mimi. Wao na watoto wao watanusurika katika hatari nao watarudi.
And I will sowe them among the people, and they shall remember me in farre countreys: and they shall liue with their children and turne againe.
10 Nitawarudisha kutoka Misri na kuwakusanya toka Ashuru. Nitawaleta katika nchi ya Gileadi na Lebanoni, na hapo hapatakuwa na nafasi ya kuwatosha.
I will bring them againe also out of the land of Egypt, and gather them out of Asshur: and I will bring them into the land of Gilead, and Lebanon, and place shall not be found for them.
11 Watapita katika bahari ya mateso; bahari iliyochafuka itatulizwa na vilindi vyote vya Mto Naili vitakauka. Kiburi cha Ashuru kitashushwa, nayo fimbo ya utawala ya Misri itatoweka.
And he shall goe into the sea with affliction, and shall smite the waues in the sea, and all the depthes of the riuer shall drye vp: and the pride of Asshur shall be cast downe, and the scepter of Egypt shall depart away.
12 Nitawaimarisha katika Bwana, na katika jina lake watatembea,” asema Bwana.
And I will strengthen them in the Lord, and they shall walke in his Name, sayth the Lord.

< Zekaria 10 >