< Zekaria 1 >

1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
In the eiythe monethe, in the secounde yeer of Darius, the word of the Lord was maad to Sacarie, the sone of Barachie, the sone of Addo,
2 “Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
profete, and seide, The Lord is wrooth on youre fadris with wrathfulnesse.
3 Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And thou schalt seie to hem, The Lord of oostis seith these thingis. Be ye conuertid to me, seith the Lord of oostis, and Y schal be conuertid to you, seith the Lord of oostis.
4 Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
Be ye not as youre fadris, to whiche the formere profetis crieden, seiynge, The Lord of oostis seith these thingis, Be ye conuertid fro youre yuel weies, and youre worste thouytis; and thei herden not, nether token tent to me, seith the Lord of oostis.
5 Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
Where ben youre fadris and profetis? whether thei schulen lyue with outen ende?
6 Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
Netheles my wordis and my lawful thingis, whiche Y comaundide to my seruauntis profetis, whether thei tauyten not youre fadris? And thei weren conuertid, and seiden, As the Lord of oostys thouyte for to do to vs bi oure weies, and bi oure fyndingis he dide to vs.
7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
In the foure and twentithe dai of the enleuenthe monethe Sabath, in the secounde yeer of Darius, the word of the Lord was maad to Sacarie, sone of Barachie, sone of Addo,
8 Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
profete, and seide, Y saiy bi niyt, and lo! a man stiynge on a reed hors; and he stood bitwixe places where mirtis wexen, that weren in the depthe, and aftir hym weren horsis reede, dyuerse, and white.
9 Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
And Y seide, My lord, who ben these? And an aungel of the Lord seide to me, that spak in me, Y schal schewe to thee what these ben.
10 Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
And the man that stood bitwix places where mirtis wexen, answeride, and seide, These it ben, whiche the Lord sente, that thei walke thorouy erthe.
11 Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
And thei answeriden to the aungel of the Lord, that stood bitwixe places where mirtis wexen, and seiden, We han walkid thorouy erthe, and lo! al erthe is enhabitid, and restith.
12 Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
And the aungel of the Lord answeride, and seide, Lord of oostis, hou long schalt thou not haue merci on Jerusalem, and citees of Juda, to whiche thou art wrooth? This now is the seuentithe yeer.
13 Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
And the Lord answeride to the aungel, that spak in me, goode wordis, and wordis of coumfort.
14 Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
And the aungel that spak in me, seide to me, Crie thou, seiynge, The Lord of oostis seith these thingis, Y louyde Jerusalem and Sion in greet feruour;
15 lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
and in greet wraththe Y schal be wroth on riche folkis; for Y was wrooth a litil, forsothe thei helpiden in to yuel.
16 “Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Therfor the Lord seith these thingis, Y schal turne ayen to Jerusalem in mercies. Myn hous schal be bildid in it, seith the Lord of oostis; and a plomet schal be streiyt out on Jerusalem.
17 “Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
Yit crie thou, seiynge, The Lord of oostis seith these thingis, Yit my citees schulen flete with goodis, and yit the Lord schal coumforte Sion, and yit he schal chese Jerusalem.
18 Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
And Y reiside myn iyen, and Y saiy, and lo! foure hornes.
19 Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
And Y seide to the aungel that spak in me, What ben these? And he seide to me, These ben hornes, that wyndewiden Juda, and Israel, and Jerusalem.
20 Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
And the Lord schewide to me foure smythis.
21 Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”
And Y seide, What comen these for to do? Which spak, seiynge, These ben the hornes, that wyndewiden Juda bi alle men, and no man of hem reiside his heed; and these camen for to make hem aferd, that thei caste doun the hornes of hethene men, which reisiden horn on the lond of Juda, for to scatere it.

< Zekaria 1 >