< Zekaria 1 >

1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
In the eighth month in the second year of Darius, this message of the Lord came to the prophet Zechariah, the son of Berechiah, the son of Iddo:
2 “Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
The Lord was furious with your ancestors.
3 Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
So tell the people this message of the Lord of hosts: “Return to me,” says the Lord of hosts, “and I will return to you” says the Lord of hosts.
4 Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
“Do not be like your ancestors to whom the former prophets cried, ‘The Lord of hosts says to turn now from your evil ways, and from your evil deeds’. They did not heed nor listen to me,” says the Lord.
5 Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
“Your ancestors, where are they? And the prophets, do they live forever?
6 Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
But did not my words and my statutes with which I charged my servants the prophets overtake your ancestors? And they repented and said, ‘Just as the Lord of hosts planned to do to us, according to our ways, and according to our deeds, so he has dealt with us.’”
7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
In the twenty-fourth day of the eleventh month, which is the month Shebat, in the second year of Darius, this message of the Lord came to the prophet Zechariah, the son of Berechiah, the son of Iddo:
8 Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
I saw in the night a man on a red horse, among the myrtle trees that were in the valley-bottom. Behind him there were horses, red, sorrel, and white.
9 Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
Then said I, “My Lord, what are these?” And the messenger who was talking with me said, “I will show you what they are.”
10 Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
And the man who was standing among the myrtle trees answered, “They are those whom the Lord has sent to patrol the earth.”
11 Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
And the riders answered the messenger of the Lord who was standing among the myrtle trees, “We have gone up and down through the world and behold, all the earth is still and at peace.”
12 Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
Then the messenger of the Lord said, “Lord of hosts, how long will you have no pity for Jerusalem and the cities of Judah with which you have been angry for seventy years?”
13 Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
And the Lord answered the messenger who was talking with me with kind and comforting words.
14 Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
So the messenger who was talking with me said to me, “Proclaim now that the Lord of hosts says: I am deeply concerned for Jerusalem.
15 lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
But I am deeply angry with the arrogant, complacent nations. I was only a little angry with Israel but they made the suffering worse.
16 “Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Therefore, says the Lord, I am turning to show mercy to Jerusalem. My temple will be rebuilt in it, says the Lord of hosts, and a measuring line will be stretched over Jerusalem.
17 “Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
Proclaim again: Thus says the Lord of hosts: My cities will again overflow with prosperity and the Lord will again comfort Zion and choose Jerusalem.”
18 Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
Now I looked up and saw four horns.
19 Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
I said to the messenger who was talking with me, “What are these?” He answered, “These are the horns which scattered Judah, Israel and Jerusalem.”
20 Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
Then the Lord showed me four smiths.
21 Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”
I said, “What are these coming to do?” He answered, “The horns scattered Judah, so that no one dared lift their head. But the smiths have come to terrify them, to crush the horns of the nations which lifted up their horn against the land of Judah to scatter its people.”

< Zekaria 1 >