< Zekaria 1 >
1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
In the eighth month, in the second year of Darius, came the word of Jehovah to Zechariah, the son of Barachiah, the son of Iddo, the prophet, saying: —
2 “Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
Jehovah hath been much displeased with your fathers.
3 Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
But say thou to them, Thus saith Jehovah of hosts: Turn ye to me, saith Jehovah of hosts, And I will turn to you, saith Jehovah of hosts.
4 Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
Be ye not as your fathers, to whom the former prophets cried, saying, Turn ye now from your evil ways, and from your evil doings! But they did not hear, nor hearken to me, saith Jehovah.
5 Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
Your fathers, where are they? And the prophets, do they live forever?
6 Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
But my words and my statutes, Which I commanded my servants, the prophets, Did they not overtake your fathers? And they returned and said, Even as Jehovah of hosts thought To do to us according to our ways, and according to doings, So hath he done to us.
7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
On the four and twentieth day of the eleventh month, which is the month Sebat, in the second year of Darius, came the word of Jehovah to Zechariah, the son of Barachiah, the son of Iddo, the prophet, saying:
8 Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
I saw in the night, and behold, a man riding upon a red horse; and he stood among the myrtle-trees that were in the deep valley, and behind him were other horses, red, fox-colored, and white.
9 Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
Then I said, What are these, my lord? And the angel that talked with me said to me, I will show thee what these are.
10 Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
And the man that stood among the myrtle-trees answered and said, These are they whom Jehovah hath sent to go to and fro through the earth.
11 Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
And they answered the angel of Jehovah that stood among the myrtle-trees, and said, We have gone to and fro through the earth, and behold, all the earth is still and at rest.
12 Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
Then the angel of Jehovah answered, and said, O Jehovah of hosts, how long wilt thou not have mercy on Jerusalem and the cities of Judah, against which thou hast had indignation these threescore and ten years?
13 Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
And Jehovah answered the angel that talked with me good words and comfortable words.
14 Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
And the angel who talked with me said to me: Proclaim thou and say, Thus saith Jehovah of hosts: I am jealous for Jerusalem and for Zion with great jealousy,
15 lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
And with great anger am I angry with the nations that are at ease; For I was but a little displeased, And they helped forward the affliction.
16 “Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Therefore thus saith Jehovah: I return to Jerusalem with mercies; My house shall be built in it, Saith Jehovah of hosts, And a measuring-line shall be stretched forth over Jerusalem.
17 “Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
Proclaim yet and say, Thus saith Jehovah of hosts: My cities shall yet overflow with prosperity, And Jehovah will yet comfort Zion, And will yet choose Jerusalem.
18 Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
Then I lifted up my eyes and looked, and behold, four horns.
19 Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
And I said to the angel that talked with me, What mean these? And he answered me, These are the horns which have scattered Judah, Israel, and Jerusalem.
20 Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
And Jehovah showed me four smiths.
21 Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”
Then said I, What come these to do? And he spake, saying, These are the horns which scattered Judah, so that no man lifted up his head; and now these are come to terrify them, to cast out the horns of the nations which lifted up their horn against the land of Judah to scatter it.