< Zekaria 1 >

1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
Měsíce osmého, léta druhého Dariova, stalo se slovo Hospodinovo k Zachariášovi synu Barachiáše, syna Iddova, proroku, řkoucí:
2 “Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
Rozhněval se Hospodin na otce vaše velice.
3 Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Protož rci těmto: Takto praví Hospodin zástupů: Navraťte se ke mně, praví Hospodin zástupů, a navrátím se k vám, praví Hospodin zástupů.
4 Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
Nebuďte jako otcové vaši, na něž volávali proroci onino předešlí, říkajíce: Takto praví Hospodin zástupů: Navraťte se nyní od cest svých zlých, i od skutků vašich zlých, ale neuposlechli, ani pozorovali mne, praví Hospodin.
5 Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
Otcové vaši kde jsou? A proroci ti zdali na věky živi jsou?
6 Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
Ale však slova má a soudové moji, kteréž jsem přikázal služebníkům svým prorokům, zdali nepostihli otců vašich? tak že obrátivše se, řekli: Jakž uložil Hospodin zástupů učiniti nám podlé cest našich, a podlé skutků našich, tak učinil nám.
7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
Dne čtyřmecítmého, jedenáctého měsíce, kterýž jest měsíc Šebat, léta druhého Dariova, stalo se slovo Hospodinovo k Zachariášovi synu Barachiáše, syna Iddova, proroku, řkoucí:
8 Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
Viděl jsem v noci, a aj, muž sedí na koni ryzím, kterýž stál mezi myrtovím, kteréž bylo v dolině, za ním pak koně ryzí, strakaté a bílé.
9 Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
I řekl jsem: Kdo jsou tito, Pane můj? Řekl mi anděl ten, kterýž mluvil se mnou: Já ukáži tobě, kdo jsou tito.
10 Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
Tedy odpovídaje muž ten, kterýž stál mezi myrtovím, řekl: Tito jsou, kteréž poslal Hospodin, aby zchodili zemi.
11 Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
I odpověděli andělu Hospodinovu tomu, kterýž stál mezi myrtovím, a řekli: Zchodili jsme zemi, a aj, všecka země bezpečně bydlí, a pokoje užívá.
12 Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
Tedy odpověděl anděl Hospodinův a řekl: Ó Hospodine zástupů, až dokudž ty se nesmiluješ nad Jeruzalémem a nad městy Judskými, na kteréž jsi hněval se již sedmdesáte let?
13 Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
I odpověděl Hospodin andělu tomu, kterýž mluvil se mnou, slovy dobrými, slovy potěšitelnými.
14 Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
Tedy řekl mi anděl, kterýž mluvil ke mně: Volej a rci: Takto praví Hospodin zástupů: Horlím pro Jeruzalém a Sion horlením velikým.
15 lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
A hněvám se náramně na ty národy, kteříž mají pokoj; nebo když jsem já se málo rozhněval, oni pomáhali k zlému.
16 “Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Protož takto praví Hospodin: Navrátil jsem se k Jeruzalému milosrdenstvím, dům můj staven bude v něm, praví Hospodin zástupů, a pravidlo vztaženo bude na Jeruzalém.
17 “Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
Ještě volej a rci: Takto praví Hospodin zástupů: Ještěť se rozsadí města má pro hojnost dobrého; neboť utěší ještě Hospodin Sion, a vyvolí ještě Jeruzalém.
18 Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
Tedy pozdvihl jsem očí svých, a uzřel jsem, a aj, čtyři rohové.
19 Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
I řekl jsem andělu, kterýž mluvil se mnou: Co jest toto? I řekl mi: To jsou ti rohové, kteříž zmítali Judou, Izraelem a Jeruzalémem.
20 Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
Ukázal mi také Hospodin čtyři kováře.
21 Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”
I řekl jsem: Co jdou dělati tito? I mluvil, řka: Tito jsou rohové, kteříž zmítali Judou, tak že žádný nemohl pozdvihnouti hlavy své. Protož přišli tito, aby je přestrašili, a srazili rohy těch národů, kteříž pozdvihli rohu proti zemi Judské, aby ní zmítali.

< Zekaria 1 >