< Tito 1 >
1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa:
Pavel, Božji služabnik in apostol Jezusa Kristusa, glede na vero Božjih izvoljencev in priznavanje resnice, ki je po bogaboječnosti;
2 imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios )
v upanju večnega življenja, ki ga je Bog, ki ne more lagati, obljubil, preden je svet nastal; (aiōnios )
3 naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:
toda ob primernih časih je svojo besedo jasno pokazal prek oznanjevanja, ki mi je bila zaupana glede na zapoved Boga, našega Odrešenika;
4 Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote: Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
Titu, mojemu lastnemu sinu, po skupni veri: ›Milost, usmiljenje in mir od Boga Očeta in Gospoda Jezusa Kristusa, našega Odrešenika.‹
5 Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza.
Na Kreti sem te pustil zaradi tega razloga, da urediš stvari, ki so pomanjkljive, ter v vsakem mestu določiš starešine, kakor sem ti določil;
6 Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi.
če je kdorkoli brez krivde, soprog ene žene, z zvestimi otroki, [ki] niso obtoženi razgrajanja ali neposlušnosti.
7 Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali.
Kajti duhovni nadzornik mora biti brez krivde, kakor Božji oskrbnik, ne samovoljen, ne hitro jezen, ne vdan vinu, ne razuzdanec, ne vdan umazani grabežljivosti;
8 Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake.
temveč ima rad gostoljubnost, ima rad dobre ljudi, trezen, pravičen, svet, zmeren;
9 Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.
ki trdno drži zvesto besedo, kakor je bil poučen, da bo lahko zmožen z zdravim naukom ugovarjalce tako spodbujati kakor prepričevati.
10 Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara.
Kajti mnogo je neposlušnih in praznih blebetačev ter sleparjev, posebno tistih iz obreze,
11 Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu.
katerih usta se morajo zapreti, ki zaradi umazanega dobička spodkopavajo cele družine, ko učijo stvari, ki jih ne bi smeli.
12 Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.”
Eden izmed njih, njihov lastni prerok, je rekel: »Krečani so vedno lažnivci, zle živali, počasni trebuhi.«
13 Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani,
To pričevanje je resnično. Zatorej jih ostro oštej, da bodo lahko zdravi v veri;
14 ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli.
ne dajajoč pozornosti judovskim bajkam in človeškim zapovedim, ki odvračajo od resnice.
15 Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka.
Čistim so vse stvari čiste, toda tem, ki so omadeževani in neverni, ni nič čisto, temveč so omadeževane celó njihove misli in vest.
16 Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.
Izpovedujejo, da poznajo Boga, toda z deli ga zanikajo, ker so gnusni in neposlušni in neuporabni za vsako dobro delo.