< Tito 1 >
1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa:
Od Pavla, sluge Božijega, a apostola Isusa Hrista po vjeri izbranijeh Božijih, i po poznanju istine pobožnosti,
2 imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios )
Za nad vjeènoga života, koji obeæa nelažni Bog prije vremena vjeènijeh, (aiōnios )
3 naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:
A javi u vremena svoja rijeè svoju propovijedanjem, koje je meni povjereno po zapovijesti spasitelja našega Boga,
4 Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote: Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
Titu, pravome sinu po vjeri nas obojice, blagodat, milost, mir od Boga oca i Gospoda Isusa Hrista, spasa našega.
5 Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza.
Zato te ostavih u Kritu da popraviš što je nedovršeno, i da postaviš po svijem gradovima sveštenike, kao što ti ja zapovjedih,
6 Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi.
Ako je ko bez mane, jedne žene muž, i ima vjernu djecu, koju ne kore za kurvarstvo ili za nepokornost.
7 Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali.
Jer vladika treba da je bez mane, kao Božij pristav; ne koji sebi ugaða, ne gnjevljiv, ne pijanica, ne bojac, ne lakom na pogani dobitak;
8 Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake.
Nego gostoljubiv, blag, pošten, pravedan, svet, èist;
9 Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.
Koji se drži vjerne rijeèi po nauci, da bude kadar i svjetovati sa zdravom naukom, i pokarati one koji se protive.
10 Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara.
Jer ima mnogo neposlušnijeh, praznogovorljivijeh, i umom prevarenijeh, a osobito koji su iz obrezanja,
11 Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu.
Kojima treba usta zatvoriti; koji cijele kuæe izopaèuju uèeæi što ne treba, poganoga dobitka radi.
12 Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.”
A reèe neko od njih, njihov prorok: Kriæani svagda lažljivi, zli zvjerovi, besposleni trbusi.
13 Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani,
Svjedoèanstvo je ovo istinito; zaradi toga uzroka karaj ih bez šteðenja, da budu zdravi u vjeri,
14 ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli.
Ne slušajuæi Jevrejskijeh gatalica ni zapovijesti ljudi koji se odvraæaju od istine.
15 Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka.
Èistima je sve èisto; a poganima i nevjernima ništa nije èisto, nego je opoganjen njihov i um i savjest.
16 Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.
Govore da poznaju Boga, a djelima ga se odrièu; jer su mrski i neposlušni, i ni za kakvo dobro djelo valjani.