< Tito 1 >

1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa:
Poul, the seruaunt of God, and apostle of Jhesu Crist, bi the feith of the chosun of God, and bi the knowing of the treuthe, whiche is aftir pitee,
2 imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios g166)
in to the hope of euerlastinge lijf, which lijf God that lieth not, bihiyte bifore tymes of the world; (aiōnios g166)
3 naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:
but he hath schewid in hise tymes his word in preching, that is bitakun to me bi the comaundement of `God oure sauyour,
4 Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote: Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
to Tite, most dereworthe sone bi the comyn feith, grace and pees of God the fadir, and of Crist Jhesu, oure sauyour.
5 Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza.
For cause of this thing Y lefte thee at Crete, that thou amende tho thingis that failen, and ordeyne preestis bi citees, as also Y disposide to thee.
6 Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi.
If ony man is withoute cryme, an hosebonde of o wijf, and hath feithful sones, not in accusacioun of letcherie, or not suget.
7 Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali.
For it bihoueth a bischop to be without cryme, a dispendour of God, not proud, not wrathful, not drunkelew, not smytere, not coueytouse of foul wynnyng;
8 Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake.
but holdinge hospitalite, benygne, prudent, sobre, iust,
9 Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.
hooli, contynent, takinge that trewe word, that is aftir doctryn; that he be miyti to amoneste in hoolsum techyng, and to repreue hem that ayenseien.
10 Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara.
For ther ben many vnobedient, and veyn spekeris, and disseyueris, moost thei that ben of circumcisyoun,
11 Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu.
whiche it bihoueth to be repreued; whiche subuerten alle housis, techinge whiche thingis it bihoueth not, for the loue of foul wynnyng.
12 Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.”
And oon of hem, her propre profete, seide, Men of Crete ben euere more lyeris, yuele beestis, of slowe wombe.
13 Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani,
This witnessyng is trewe. For what cause blame hem sore, that thei be hool in feith,
14 ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli.
not yyuynge tent to fablis of Jewis, and to maundementis of men, that turnen awei hem fro treuthe.
15 Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka.
And alle thingis ben clene to clene men; but to vnclene men and to vnfeithful no thing is clene, for the soule and conscience of hem ben maad vnclene.
16 Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.
Thei knoulechen that thei knowen God, but bi dedis thei denyen; whanne thei ben abhominable, and vnbileueful, and repreuable to al good werk.

< Tito 1 >