< Tito 1 >

1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa:
Paul a servant of God, and an apostle of Jesus Christ, for promoting the faith of God's chosen people, and the knowledge of the truth which is according to godliness:
2 imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios g166)
in hope of eternal life, which God, who cannot lie, promised before all ages; (aiōnios g166)
3 naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:
and hath in his own times manifested his word, by the preaching, with which I was intrusted according to the commandment of God our Saviour:
4 Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote: Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
to Titus my son in the common faith, grace, mercy, and peace from God the Father, and the Lord Jesus Christ our Saviour.
5 Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza.
For this cause I left thee in Crete, that thou mightest set in order what remained, and ordain elders in every city as I directed thee:
6 Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi.
to wit, if any one be blameless, the husband of one wife, having faithful children, not accused of debauchery, or unruly.
7 Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali.
For a bishop must be blameless as the steward of God, not self-willed, not passionate, not given to wine, no striker, not greedy of sordid gain:
8 Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake.
but hospitable, benevolent, sober, just, holy, temperate;
9 Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.
holding fast the faithful word, according as he hath been taught, that he may be able both to instruct in sound doctrine, and to convince gainsayers.
10 Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara.
For there are many disorderly persons, vain-talkers and deceivers, especially those of the circumcision; whose mouths must be stopped:
11 Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu.
who subvert whole families, teaching what they ought not, for shameful gain:
12 Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.”
as said one of themselves, a prophet of their own, "The Cretans are always liars, mischievous beasts, sluggish gluttons."
13 Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani,
This testimony is true: for which cause rebuke them sharply, that they may be found in the faith;
14 ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli.
not attending to Jewish fables, and the precepts of men who turn away from the truth.
15 Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka.
To the pure indeed all things are pure; but to the polluted and unbelieving nothing is pure; even their mind and conscience is polluted.
16 Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.
They profess to know God, but in works deny Him, being abominable and disobedient, and to every thing that is good void of understanding.

< Tito 1 >