< Tito 1 >

1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa:
Paul, the servant of God, and apostle of Jesus Christ, according to the faith of the elect of God, and the perfect knowledge of the truth which is according to godliness,
2 imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios g166)
in the hope of eternal life, which God who cannot lie, promised before the eternal times, (aiōnios g166)
3 naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:
and manifested in his own seasons his word by preaching, with which I am intrusted, according to the commandment of God our Saviour;
4 Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote: Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
to Titus, my beloved son according to the common faith. Grace and peace from God the Father and Jesus Christ our Saviour.
5 Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza.
Therefore I left you in Crete, in order that you may set in order remaining things, and establish elders in every city, as I commanded you;
6 Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi.
if any one is irreproachable, the husband of one wife, having faithful children, not in accusation of riot or incorrigible.
7 Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali.
For it behooves the bishop to be blameless, as the steward of God; not audacious, not irascible, not given to wine, not a controvertist, not fond of filthy lucre;
8 Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake.
but hospitable, loving the good, prudent, righteous, holy, temperate;
9 Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.
holding that which is according to the teaching of the faithful word, in order that he may be able both to exhort with healthy teaching, and to convict the opposers.
10 Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara.
For many are incorrigible, speaking vain things and egotistical, especially those from the circumcision,
11 Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu.
whose mouths it is necessary to stop; who overturn whole families, teaching those things which it does not behoove, for the sake of disgraceful gain.
12 Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.”
A certain one of them, their own prophet, said, The Cretans are all liars, evil beasts, slow stomachs.
13 Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani,
This testimony is true: on account of which cause convict them sharply, in order that they may be sound in the faith,
14 ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli.
not giving heed to Jewish fables, and commandments of men turning away from the truth.
15 Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka.
To the pure all things are pure: but to the corrupted and unbelieving there is nothing pure; yea, their mind and their conscience are polluted.
16 Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.
They profess to know God, but deny him by their works, being abominable, and unbelieving, and reprobate unto every good work.

< Tito 1 >