< Tito 3 >

1 Wakumbushe watu kuwanyenyekea watawala na kuwatii wenye mamlaka, wawe tayari kutenda kila lililo jema.
Admonish them to be submissive to governors and magistrates, to obey their orders, and to be ready to every good work;
2 Wasimnenee mtu yeyote mabaya, wasiwe wagomvi, bali wawe wapole, wakionyesha unyenyekevu kwa watu wote.
to slander no man, to avoid contention, to be gentle, shewing all meekness unto all men.
3 Maana sisi wenyewe wakati fulani tulikuwa wajinga, wasiotii, tukiwa watumwa wa tamaa mbaya na anasa za kila aina. Tuliishi katika uovu na wivu, tukichukiwa na kuchukiana sisi kwa sisi.
For we also were formerly foolish, disobedient, going astray, enslaved to various disorderly appetites and pleasures, living in malice and envy, hateful, and hating one another.
4 Lakini wema na upendo wa Mungu Mwokozi wetu ulipofunuliwa,
But when the kindness and love of God our Saviour towards man appeared,
5 alituokoa, si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya rehema zake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa mara ya pili na kwa kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu,
not for works of righteousness which we had done, but according to his own mercy He saved us, by the washing of regeneration, and renewing of the holy Spirit;
6 ambaye Mungu alitumiminia kwa wingi kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu,
which He hath plentifully shed upon us, through Jesus Christ our Saviour:
7 ili kwamba, tukiisha kuhesabiwa haki kwa neema yake, tupate kuwa warithi tukiwa na tumaini la uzima wa milele. (aiōnios g166)
that being justified by his grace, we might become heirs according to the hope of eternal life. (aiōnios g166)
8 Hili ni neno la kuaminiwa. Nami nataka uyasisitize mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu wapate kuwa waangalifu kujitoa kwa ajili ya kutenda mema wakati wote. Mambo haya ni mazuri tena ya manufaa kwa kila mtu.
This is a word which ought to believed and observed, and concerning these things I would have thee stedfastly affirm, that they who have believed in God be careful to excel in good works: for these things are good and profitable to men.
9 Lakini jiepushe na maswali ya kipuzi, mambo ya koo, mabishano na ugomvi kuhusu sheria, kwa sababu hayana faida, tena ni ubatili.
But avoid foolish questions, and genealogies, and strifes and contentions about the law; for they are unprofitable and vain:
10 Mtu anayesababisha mafarakano, mwonye mara ya kwanza, kisha mwonye mara ya pili. Baada ya hapo, usihusike naye tena.
reject therefore such an heretical man, after the first and second admonition; knowing that such a one is perverted,
11 Kwa kuwa unajua kwamba mtu kama huyo amepotoka na tena ni mwenye dhambi. Yeye amejihukumu mwenyewe.
and sinneth as being self-condemned.
12 Mara nitakapomtuma Artema au Tikiko kwako, jitahidi kuja unione huko Nikopoli, kwa sababu nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
When I shall send Artemas to thee, or Tychicus, endeavour to come to me to Nicopolis: for there I have determined to winter.
13 Fanya kila uwezalo uwasafirishe Zena yule mwanasheria na Apolo na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji katika safari yao.
Forward Zenas the lawyer, and Apollos, on their journey carefully, that nothing may be wanting to them.
14 Watu wetu hawana budi kujifunza kutenda mema, ili waweze kuyakimu mahitaji ya kila siku, wasije wakaishi maisha yasiyokuwa na matunda.
And let our brethren-also learn to excel in good works for necessary exigencies, that they may not be unfruitful.
15 Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale wanaotupenda katika imani. Neema iwe nanyi nyote. Amen.
All that are with me salute thee. Salute them that love us in the faith. Grace be with you all. Amen.

< Tito 3 >