< Tito 3 >

1 Wakumbushe watu kuwanyenyekea watawala na kuwatii wenye mamlaka, wawe tayari kutenda kila lililo jema.
Remind them to submit to rulers and authorities, to obey them, to be ready for every good work,
2 Wasimnenee mtu yeyote mabaya, wasiwe wagomvi, bali wawe wapole, wakionyesha unyenyekevu kwa watu wote.
to revile no one, to not be eager to fight, and to be gentle, showing all humility toward everyone.
3 Maana sisi wenyewe wakati fulani tulikuwa wajinga, wasiotii, tukiwa watumwa wa tamaa mbaya na anasa za kila aina. Tuliishi katika uovu na wivu, tukichukiwa na kuchukiana sisi kwa sisi.
For once we ourselves were thoughtless and disobedient. We were led astray and enslaved by various passions and pleasures. We lived in evil and envy. We were detestable and hated one another.
4 Lakini wema na upendo wa Mungu Mwokozi wetu ulipofunuliwa,
But when the kindness of God our savior and his love for mankind appeared,
5 alituokoa, si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya rehema zake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa mara ya pili na kwa kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu,
it was not by works of righteousness that we did, but by his mercy that he saved us. He saved us through the washing of new birth and renewal by the Holy Spirit.
6 ambaye Mungu alitumiminia kwa wingi kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu,
God richly poured the Holy Spirit on us through our Savior Jesus Christ,
7 ili kwamba, tukiisha kuhesabiwa haki kwa neema yake, tupate kuwa warithi tukiwa na tumaini la uzima wa milele. (aiōnios g166)
so that having been justified by his grace, we might become heirs with the certain hope of eternal life. (aiōnios g166)
8 Hili ni neno la kuaminiwa. Nami nataka uyasisitize mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu wapate kuwa waangalifu kujitoa kwa ajili ya kutenda mema wakati wote. Mambo haya ni mazuri tena ya manufaa kwa kila mtu.
This message is trustworthy. I want you to insist on these things, so that those who have believed in God may be careful to engage themselves in good works. These things are good and useful for everyone.
9 Lakini jiepushe na maswali ya kipuzi, mambo ya koo, mabishano na ugomvi kuhusu sheria, kwa sababu hayana faida, tena ni ubatili.
But avoid foolish debates and genealogies and strife and conflict about the law. Those things are unprofitable and worthless.
10 Mtu anayesababisha mafarakano, mwonye mara ya kwanza, kisha mwonye mara ya pili. Baada ya hapo, usihusike naye tena.
Reject anyone who is causing divisions among you, after one or two warnings,
11 Kwa kuwa unajua kwamba mtu kama huyo amepotoka na tena ni mwenye dhambi. Yeye amejihukumu mwenyewe.
knowing that such a person has turned from the right way and is sinning and condemns himself.
12 Mara nitakapomtuma Artema au Tikiko kwako, jitahidi kuja unione huko Nikopoli, kwa sababu nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
When I send Artemas or Tychicus to you, hurry and come to me at Nicopolis, where I have decided to spend the winter.
13 Fanya kila uwezalo uwasafirishe Zena yule mwanasheria na Apolo na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji katika safari yao.
Do everything you can to send on their way Zenas the lawyer and Apollos, so that they lack nothing.
14 Watu wetu hawana budi kujifunza kutenda mema, ili waweze kuyakimu mahitaji ya kila siku, wasije wakaishi maisha yasiyokuwa na matunda.
Our people must learn to engage themselves in good works that provide for urgent needs, and so not be unfruitful.
15 Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale wanaotupenda katika imani. Neema iwe nanyi nyote. Amen.
All those who are with me greet you. Greet those who love us in faith. Grace be with all of you.

< Tito 3 >