< Tito 3 >

1 Wakumbushe watu kuwanyenyekea watawala na kuwatii wenye mamlaka, wawe tayari kutenda kila lililo jema.
Put them in mind that to princes and to powers they are to hearken and to be obedient, and to be prepared for every good work.
2 Wasimnenee mtu yeyote mabaya, wasiwe wagomvi, bali wawe wapole, wakionyesha unyenyekevu kwa watu wote.
And against no man to rail, nor be contentious, but gentle, and in every thing to show their benignity towards all men.
3 Maana sisi wenyewe wakati fulani tulikuwa wajinga, wasiotii, tukiwa watumwa wa tamaa mbaya na anasa za kila aina. Tuliishi katika uovu na wivu, tukichukiwa na kuchukiana sisi kwa sisi.
For we also were afore-time without understanding, and disobedient and erring, and were subjected to various lusts; and in malice, and in envy we conversed, and were hateful, and also hating one another.
4 Lakini wema na upendo wa Mungu Mwokozi wetu ulipofunuliwa,
But when appeared the goodness and mercy of Aloha our Saviour,
5 alituokoa, si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya rehema zake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa mara ya pili na kwa kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu,
not by works of righteousness which we had done, but by his own mercy he saved us, by the laving of the birth which is afresh, by the renewing of the Spirit of Holiness,
6 ambaye Mungu alitumiminia kwa wingi kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu,
which he shed upon us abundantly, by Jeshu Meshiha our Saviour;
7 ili kwamba, tukiisha kuhesabiwa haki kwa neema yake, tupate kuwa warithi tukiwa na tumaini la uzima wa milele. (aiōnios g166)
that by his grace we might be justified, and be made heirs according to the hope of the life which is eternal. (aiōnios g166)
8 Hili ni neno la kuaminiwa. Nami nataka uyasisitize mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu wapate kuwa waangalifu kujitoa kwa ajili ya kutenda mema wakati wote. Mambo haya ni mazuri tena ya manufaa kwa kila mtu.
Faithful is the word; and in this I will that thou also establish them, that they should be careful to perform good works, they who have believed in Aloha. These are good and profitable unto men.
9 Lakini jiepushe na maswali ya kipuzi, mambo ya koo, mabishano na ugomvi kuhusu sheria, kwa sababu hayana faida, tena ni ubatili.
But from foolish disputations, and from tales of genealogies, and from contentions, and strifes of the sophree, withdraw; for profit is not in them, and they are vain.
10 Mtu anayesababisha mafarakano, mwonye mara ya kwanza, kisha mwonye mara ya pili. Baada ya hapo, usihusike naye tena.
From an heretical man, after one time and twice thou hast admonished him, withdraw;
11 Kwa kuwa unajua kwamba mtu kama huyo amepotoka na tena ni mwenye dhambi. Yeye amejihukumu mwenyewe.
and know that he who is such is perverse, and sinneth, and condemneth himself.
12 Mara nitakapomtuma Artema au Tikiko kwako, jitahidi kuja unione huko Nikopoli, kwa sababu nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
When I have sent to thee Artema, or Tykikos, be careful to come to me at Nikopolis; for there I have determined in my mind to winter.
13 Fanya kila uwezalo uwasafirishe Zena yule mwanasheria na Apolo na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji katika safari yao.
But concerning Zina the sophra, and Apolo, be careful to provide them well, that nothing may be wanting to them.
14 Watu wetu hawana budi kujifunza kutenda mema, ili waweze kuyakimu mahitaji ya kila siku, wasije wakaishi maisha yasiyokuwa na matunda.
And let those also who are of us, learn to perform good works in things which are necessary, that they may not be without fruits.
15 Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale wanaotupenda katika imani. Neema iwe nanyi nyote. Amen.
All they who are with me ask for thy peace. Ask for the peace of all who love us in the faith. Grace be with all of you. Amen.

< Tito 3 >