< Tito 3 >

1 Wakumbushe watu kuwanyenyekea watawala na kuwatii wenye mamlaka, wawe tayari kutenda kila lililo jema.
Påmind dem om at underordne sig Øvrigheder og Myndigheder, at adlyde, at være redebonne til al god Gerning.
2 Wasimnenee mtu yeyote mabaya, wasiwe wagomvi, bali wawe wapole, wakionyesha unyenyekevu kwa watu wote.
ikke at forhåne nogen, ikke være stridslystne, men milde, og udvise al Sagtmodighed imod alle Mennesker.
3 Maana sisi wenyewe wakati fulani tulikuwa wajinga, wasiotii, tukiwa watumwa wa tamaa mbaya na anasa za kila aina. Tuliishi katika uovu na wivu, tukichukiwa na kuchukiana sisi kwa sisi.
Thi også vi vare fordum uforstandige, ulydige, vildfarende, Slaver af Begæringer og, mange Hånde Lyster, vi levede i Ondskab og Avind, vare forhadte og hadede hverandre.
4 Lakini wema na upendo wa Mungu Mwokozi wetu ulipofunuliwa,
Men da Guds, vor Frelsers Godhed og Menneskekærlighed åbenbaredes,
5 alituokoa, si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya rehema zake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa mara ya pili na kwa kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu,
frelste han os, ikke for de Retfærdigheds Gerningers Skyld, som vi havde gjort, men efter sin Barmhjertighed, ved Igenfødelsens Bad og Fornyelsen i den Helligånd,
6 ambaye Mungu alitumiminia kwa wingi kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu,
som han rigeligt udøste over os ved Jesus Kristus, vor Frelser,
7 ili kwamba, tukiisha kuhesabiwa haki kwa neema yake, tupate kuwa warithi tukiwa na tumaini la uzima wa milele. (aiōnios g166)
for at vi, retfærdiggjorte ved hans Nåde, skulde i Håb vorde Arvinger til evigt Liv. (aiōnios g166)
8 Hili ni neno la kuaminiwa. Nami nataka uyasisitize mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu wapate kuwa waangalifu kujitoa kwa ajili ya kutenda mema wakati wote. Mambo haya ni mazuri tena ya manufaa kwa kila mtu.
Den Tale er troværdig, og derom vil jeg, at du skal forsikre dem, for at de, som ere komne til Tro på Gud, skulle lægge Vind på at øve gode Gerninger. Dette er Menneskene godt og nyttigt.
9 Lakini jiepushe na maswali ya kipuzi, mambo ya koo, mabishano na ugomvi kuhusu sheria, kwa sababu hayana faida, tena ni ubatili.
Men hold dig fra tåbelige Stridigheder og Slægtregistre og Kiv og Kampe om Loven; thi de ere unyttige og frugtesløse.
10 Mtu anayesababisha mafarakano, mwonye mara ya kwanza, kisha mwonye mara ya pili. Baada ya hapo, usihusike naye tena.
Et kættersk Menneske skal du afvise efter een og to Ganges Påmindelse,
11 Kwa kuwa unajua kwamba mtu kama huyo amepotoka na tena ni mwenye dhambi. Yeye amejihukumu mwenyewe.
da du ved, at en sådan er forvendt og synder, domfældt af sig selv.
12 Mara nitakapomtuma Artema au Tikiko kwako, jitahidi kuja unione huko Nikopoli, kwa sababu nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
Når jeg sender Artemas til dig eller Tykikus, da gør dig Flid for at komme til mig i Nikopolis; thi der har jeg besluttet at overvintre.
13 Fanya kila uwezalo uwasafirishe Zena yule mwanasheria na Apolo na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji katika safari yao.
Zenas den lovkyndige og Apollos skal du omhyggeligt hjælpe på Vej, for at intet skal fattes dem.
14 Watu wetu hawana budi kujifunza kutenda mema, ili waweze kuyakimu mahitaji ya kila siku, wasije wakaishi maisha yasiyokuwa na matunda.
Men lad også vore lære at øve gode Gerninger, hvor der er Trang dertil, for at de ikke skulle være uden Frugt.
15 Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale wanaotupenda katika imani. Neema iwe nanyi nyote. Amen.
Alle, som ere hos mig, hilse dig. Hils dem, som elske os i Troen. Nåden være med eder alle!

< Tito 3 >