< Tito 3 >

1 Wakumbushe watu kuwanyenyekea watawala na kuwatii wenye mamlaka, wawe tayari kutenda kila lililo jema.
Ba de ya bi wa ba bahtu mba nu beh chua mba wo tere mba.
2 Wasimnenee mtu yeyote mabaya, wasiwe wagomvi, bali wawe wapole, wakionyesha unyenyekevu kwa watu wote.
U ka llah ni bawu du mba na mere idi na mba kana sen iyu ni idina. du mba zo mba ni mi sisunron.
3 Maana sisi wenyewe wakati fulani tulikuwa wajinga, wasiotii, tukiwa watumwa wa tamaa mbaya na anasa za kila aina. Tuliishi katika uovu na wivu, tukichukiwa na kuchukiana sisi kwa sisi.
Na kima khi na sun ni buh na khi na kpakyeme ni kpabuna.
4 Lakini wema na upendo wa Mungu Mwokozi wetu ulipofunuliwa,
Ni toh kima Irji a ji ikpan shishi ye.
5 alituokoa, si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya rehema zake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa mara ya pili na kwa kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu,
Ana hei ni tu indu dedema wa khi ti na. irji a glata ni iyi Yesu
6 ambaye Mungu alitumiminia kwa wingi kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu,
irji a nuta Ibrji Tsra tsra gbugbuu ni tu Yesu. Wa a ye kpata chuwoa.
7 ili kwamba, tukiisha kuhesabiwa haki kwa neema yake, tupate kuwa warithi tukiwa na tumaini la uzima wa milele. (aiōnios g166)
A teenaki du khi sun kasaisai ni seisei. (aiōnios g166)
8 Hili ni neno la kuaminiwa. Nami nataka uyasisitize mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu wapate kuwa waangalifu kujitoa kwa ajili ya kutenda mema wakati wote. Mambo haya ni mazuri tena ya manufaa kwa kila mtu.
I wayi a hi ton du jaji. Mei sun du tere tere ki bei wa ba kpa Irji teh u jaji mba zere zere u dedema.
9 Lakini jiepushe na maswali ya kipuzi, mambo ya koo, mabishano na ugomvi kuhusu sheria, kwa sababu hayana faida, tena ni ubatili.
U ka domeh ni seh yun u kukulu. ni mbala gye gyere. U sun yun ni tu ibeh U Irji. Ikpi mba ki mba na no ta ipkina.
10 Mtu anayesababisha mafarakano, mwonye mara ya kwanza, kisha mwonye mara ya pili. Baada ya hapo, usihusike naye tena.
Kahme ni idi wa ani chah mba wa ana son tsrei tsrei niyi na.
11 Kwa kuwa unajua kwamba mtu kama huyo amepotoka na tena ni mwenye dhambi. Yeye amejihukumu mwenyewe.
Bika toh nji kima ana zren tsrei tsrei na.
12 Mara nitakapomtuma Artema au Tikiko kwako, jitahidi kuja unione huko Nikopoli, kwa sababu nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
Uwa me ton Artemas ka Tychikus ni wu, ndu ye gbagbla ni me ni Nicopolis ndu su son ni men.
13 Fanya kila uwezalo uwasafirishe Zena yule mwanasheria na Apolo na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji katika safari yao.
U tru Zinas gbagbla, wa a to mlazren ni Appolos ni kon wa ba he ni
14 Watu wetu hawana budi kujifunza kutenda mema, ili waweze kuyakimu mahitaji ya kila siku, wasije wakaishi maisha yasiyokuwa na matunda.
A bi duu ijinbu idi bu khi yah de te kpi dedema da yibi ulu'a ani ye gba gbla du mba na sun hlegana.
15 Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale wanaotupenda katika imani. Neema iwe nanyi nyote. Amen.
Bei wa'a ba hey ni mei mba chiu. chi bei wa'a mba kpakyeme ni ta ni mi itere u jaji. zeze i irji du sun ni yi wa wuu.

< Tito 3 >