< Tito 1 >
1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa:
Paul, a servant of God—an apostle moreover of Jesus Christ, —according to the faith of the chosen ones of God, and the personal knowledge of the truth that is according to godliness, —
2 imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios )
In hope of life age-abiding; which God, who cannot lie, promised before age-during times, (aiōnios )
3 naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:
but hath manifested in its fitting seasons, even his word, in the proclamation with which entrusted am I—by injunction of our Saviour God:
4 Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote: Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
Unto Titus, my true child according to a common faith, —favour and peace, from God [our] Father and Christ Jesus our Saviour.
5 Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza.
For this cause left I thee in Crete, that, the things remaining undone, thou mightest completely set in order, and mightest establish, in every city, elders, as, I, with thee arranged: —
6 Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi.
If anyone is unaccusable, a husband of, one wife, having children that believe, who are not charged with riotous excess, nor insubordinate;
7 Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali.
For it is needful that the overseer be—unaccusable, as God’s steward, not self-willed, not soon angry, not given to wine, not ready to wound, not seeking gain by base means,
8 Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake.
But hospitable, a lover of what is good, sober-minded, just, kind, possessing self-control,
9 Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.
Holding fast, in the matter of his teaching, the faithful word, that he may be able both to encourage with his healthful instruction, and, the gainsayers, to refute.
10 Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara.
For there are many unruly men, vain talkers and deceivers, especially they of the circumcision, —
11 Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu.
Whose mouths must needs be stopped, men who are upsetting whole houses, teaching the things which ought not [to be taught] —for the sake of base gain.
12 Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.”
Said one from among them, a prophet, of their own!—Cretans! always false, mischievous wild-beasts, idle gluttons:
13 Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani,
This witness, is true, —for which cause, be reproving them sharply, that they may be healthy in their faith,
14 ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli.
Not giving heed to Judaical stories and commandments of men who are turning away from the truth:
15 Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka.
All things, are pure, unto the pure, but, unto the polluted and faithless, nothing, is pure, but polluted are both their mind and conscience;
16 Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.
God, they confess that they know, but, by their works, they deny him, being, abominable, and obdurate, and, as to any good work, found, worthless.