< Tito 1 >

1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa:
Paul, a servant of God, and an apostle of Jesus Christ, according to the faith of the chosen ones of God, and an acknowledging of truth that [is] according to piety,
2 imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios g166)
on hope of continuous life, which God, who does not lie, promised before times of ages (aiōnios g166)
3 naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:
(and He revealed His word in [His] own times), in preaching, which I was entrusted with, according to a charge of God our Savior,
4 Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote: Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
to Titus—true child according to a common faith: Grace, [[kindness, ]] peace, from God the Father and the Lord Jesus Christ our Savior!
5 Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza.
For this cause I left you in Crete, that you may arrange the things lacking, and may set elders down in every city, as I appointed to you,
6 Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi.
if anyone is blameless, a husband of one wife, having believing children, not under accusation of riotous living or insubordinate—
7 Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali.
for it is required of the overseer to be blameless, as God’s steward, not self-pleased, nor prone to anger, not given to wine, not an abuser, not given to shameful gain,
8 Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake.
but a lover of strangers, a lover of [the] good, sober-minded, righteous, holy, self-controlled,
9 Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.
holding—according to the teaching—to the steadfast word, that he may also be able to exhort in the sound teaching, and to convict the deniers;
10 Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara.
for there are many both insubordinate, vain-talkers, and mind-deceivers—especially those of the circumcision—
11 Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu.
whose mouths must be covered, who overturn whole households, teaching what things it should not, for [the] sake of shameful gain.
12 Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.”
A certain one of them, a prophet of their own, said, “Cretans! Always liars, evil beasts, lazy bellies!”
13 Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani,
This testimony is true; for which cause convict them sharply, that they may be sound in the faith,
14 ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli.
not giving heed to Jewish fables and commands of men, turning themselves away from the truth.
15 Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka.
All things, indeed, [are] pure to the pure, and nothing [is] pure to the defiled and unsteadfast, but even the mind and the conscience of them [is] defiled.
16 Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.
They profess to know God, but they deny [Him] by their works, being abominable, and disobedient, and disapproved to every good work.

< Tito 1 >