< Tito 1 >
1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa:
Paul, a slave of God and an apostle of Jesus Christ according to the faith of God's elect and a real knowledge of the Truth that accords with godliness,
2 imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios )
in hope of eternal life—which life God, who cannot lie, promised before the ages of time (aiōnios )
3 naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:
but has manifested by a proclamation of His Word at chosen times, which word was entrusted to me by the command of our Savior God;
4 Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote: Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
to Titus, a true son in a common faith: Grace, mercy, peace, from Father God and Sovereign Jesus Christ, our Savior.
5 Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza.
I left you in Crete for this reason, that you should set in order the things that were lacking and appoint elders in every town as I directed you
6 Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi.
—if a man is blameless, a one-woman man, having children who believe and who are not open to the charge of being wild or disobedient.
7 Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali.
Because as an administrator under God the overseer must be blameless; not self-willed, not hotheaded, not given to wine, not a bully, not avaricious;
8 Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake.
but rather hospitable, a lover of what is good, prudent, just, holy, disciplined;
9 Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.
holding fast the trustworthy Word as taught, so that he may be competent both to exhort with the sound doctrine and to correct those who oppose it.
10 Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara.
Because there really are lots of rebels, loudmouths and deceivers, especially those of the circumcision group,
11 Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu.
who must be silenced—they are ruining whole households, teaching things that they ought not, and for dishonest gain!
12 Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.”
One of them, a prophet of their own, said, “Cretans are always liars, evil beasts, lazy gluttons.”
13 Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani,
This testimony is true. Therefore correct them rigorously, that they may be sound in the faith,
14 ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli.
not paying attention to Jewish fables or to commands of men who are rejecting the truth.
15 Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka.
To the pure, all things are pure, but to those who are defiled and unbelieving, nothing is pure; in fact, both their minds and their consciences are defiled.
16 Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.
They profess to know God, but by their actions they deny Him, being detestable, disobedient and disqualified for any good work.