< Tito 1 >

1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa:
Paul, a bondman of God and an apostle of Jesus Christ, according to the faith of the chosen of God, and the knowledge of truth according to piety,
2 imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios g166)
in hope of eternal life, which the non-lying God promised before times eternal, (aiōnios g166)
3 naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:
but in his own times he made known his word by preaching, which I was entrusted according to the commandment of God our Savior,
4 Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote: Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
to Titus, a genuine child according to the common faith: Grace, mercy, peace from God the Father and the Lord Jesus Christ our Savior.
5 Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza.
I left thee behind in Crete on account of this: That thou should set in order the things lacking, and appoint elders in every city as I commanded thee,
6 Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi.
if any man is blameless, the husband of one wife, having believing children, not with an accusation of debauchery or insubordinate.
7 Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali.
For the overseer must be blameless as a steward of God, not self-willed, not prone to anger, not a drunkard, not a fighter, not greedy of base gain,
8 Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake.
but a lover of strangers, a lover of good, serious minded, just, devout, self-controlled,
9 Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.
holding firm the faithful word according to the teaching, so that he may also be able to exhort by the sound doctrine, and to correct those who contradict.
10 Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara.
For there are also many insubordinate men, vain talkers and deceivers, especially those from circumcision,
11 Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu.
who must be muzzled, men who subvert whole houses, teaching things that they ought not, for sake of ugly profit.
12 Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.”
A certain man of themselves, a prophet of their own, said, Cretans are always liars, evil beasts, lazy bellies.
13 Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani,
This testimony is true, because of which reason, reprove them harshly, so that they may be sound in the faith,
14 ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli.
not giving heed to Jewish myths, and commandments of men who turn away from the truth.
15 Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka.
Truly to the pure all things are pure, but to those who are defiled and unbelieving nothing is pure, but both their mind and their conscience are defiled.
16 Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.
They profess to know God, but in their works they deny him, being abominable, and disobedient, and worthless for every good work.

< Tito 1 >