< Wimbo wa Sulemani 1 >

1 Wimbo ulio bora wa Solomoni.
Das Lied der Lieder, von Salomo.
2 Unibusu kwa busu la kinywa chako, kwa maana upendo wako unafurahisha kuliko divai.
Er küsse mich mit seines Mundes Küssen; denn lieblicher als Wein ist deine Liebe.
3 Manukato yako yananukia vizuri, jina lako ni kama manukato yaliyomiminwa. Ndiyo sababu wanawali wanakupenda!
Lieblich duften deine Salben; wie ausgegossenes Öl ist dein Name, darum haben dich Jungfrauen lieb.
4 Nichukue twende nawe, na tufanye haraka! Mfalme na anilete ndani ya vyumba vyake. Marafiki Tunakushangilia na kukufurahia, tutasifu upendo wako zaidi kuliko divai. Mpendwa Tazama jinsi ilivyo bora wakupende!
Zieh mich dir nach; o, laß uns eilen! - mich führte der König in seine Gemächer - Wir wollen jubeln und uns deiner freuen, deine Liebe preisen mehr als den Wein; mit Recht lieben sie dich!
5 Mimi ni mweusi, lakini napendeza, enyi binti za Yerusalemu, mweusi kama mahema ya Kedari, kama mapazia ya hema la Solomoni.
Schwarz bin ich, doch lieblich, ihr Töchter Jerusalems! wie Kedars Gezelte, wie Salomos Zeltdecken.
6 Usinikazie macho kwa sababu mimi ni mweusi, kwa sababu nimefanywa mweusi na jua. Wana wa mama yangu walinikasirikia na kunifanya niwe mtunza mashamba ya mizabibu. Shamba langu mwenyewe la mizabibu nimeliacha.
Seht mich nicht an, daß ich so schwärzlich bin, daß die Sonne mich verbrannt hat. Die Söhne meiner Mutter zürnten auf mich; sie bestellten mich zur Weinbergshüterin - meinen eigenen Weinberg habe ich nicht gehütet!
7 Niambie, wewe ambaye ninakupenda, unalisha wapi kundi lako la kondoo na ni wapi unapowapumzisha kondoo wako adhuhuri. Kwa nini niwe kama mwanamke aliyefunikwa shela karibu na makundi ya rafiki zako?
Thu' mir kund, o du, den meine Seele liebt: Wo weidest du? wo lagerst du am Mittag? Denn warum soll ich wie eine Vermummte sein bei den Herden deiner Genossen?
8 Kama hujui, ewe mwanamke mzuri kuliko wote, fuata nyayo za kondoo, na kulisha wana-mbuzi wako karibu na hema za wachungaji.
Wenn du's nicht weißt, o du schönste unter den Frauen, so geh' doch hinaus den Spuren der Herde nach und weide deine Zicklein bei den Hütten der Hirten.
9 Mpenzi wangu, ninakufananisha na farasi jike aliyefungwa katika mojawapo ya magari ya vita ya Farao.
Den Stuten am Pharaowagen vergleiche ich dich, meine Freundin.
10 Mashavu yako yanapendeza yakiwa na vipuli, shingo yako ikiwa na mikufu ya vito.
Lieblich stehn deinen Wangen die Gehänge, deinem Halse die Schnüre.
11 Tutakufanyia vipuli vya dhahabu, vyenye kupambwa kwa fedha.
Gehänge von Gold wollen wir dir machen mit silbernen Punkten.
12 Wakati mfalme alipokuwa mezani pake, manukato yangu yalisambaza harufu yake nzuri.
So lange der König auf seinem Ruhepolster weilte, gab meine Narde ihren Duft.
13 Mpenzi wangu kwangu mimi ni kifuko cha manemane kati ya matiti yangu.
Mein Geliebter ist mir das Balsambündel, das an meinem Busen ruht.
14 Mpenzi wangu kwangu mimi ni kama kishada cha maua ya mhina kutoka mashamba ya mizabibu ya En-Gedi.
Die Cyprusdolde in Engedis Weinbergen ist mein Geliebter mir.
15 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! Tazama jinsi ulivyo mzuri! Macho yako ni kama ya hua.
Wie schön bist du, meine Freundin; wie schön bist du! Deine Augen sind Taubenaugen.
16 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! Ee, tazama jinsi unavyopendeza! Na kitanda chetu ni cha majani mazuri.
Wie schön bist du, mein Geliebter, ja holdselig; ja immer grün ist unser Lager.
17 Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, na mapao yetu ni miberoshi.
Die Balken unseres Hauses sind Cedern, unser Getäfel Cypressen.

< Wimbo wa Sulemani 1 >