< Wimbo wa Sulemani 8 >

1 Laiti ungelikuwa kwangu kama ndugu wa kiume, ambaye aliyanyonya matiti ya mama yangu! Kisha, kama ningekukuta huko nje, ningelikubusu, wala hakuna mtu yeyote angelinidharau.
巴不得你像我的兄弟, 像吃我母亲奶的兄弟; 我在外头遇见你就与你亲嘴, 谁也不轻看我。
2 Ningelikuongoza na kukuleta katika nyumba ya mama yangu, yeye ambaye amenifundisha. Ningelikupa divai iliyokolezwa unywe, asali ya maua ya mikomamanga yangu.
我必引导你, 领你进我母亲的家; 我可以领受教训, 也就使你喝石榴汁酿的香酒。
3 Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu, na mkono wake wa kuume unanikumbatia.
他的左手必在我头下; 他的右手必将我抱住。
4 Binti za Yerusalemu, ninawaagiza: msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe.
耶路撒冷的众女子啊, 我嘱咐你们: 不要惊动、不要叫醒我所亲爱的, 等他自己情愿。
5 Ni nani huyu anayekuja kutoka nyikani akimwegemea mpenzi wake? Mpendwa Nilikuamsha chini ya mtofaa, huko mama yako alipotunga mimba yako, huko yeye alipata utungu akakuzaa.
那靠着良人从旷野上来的是谁呢? 〔新娘〕 我在苹果树下叫醒你。 你母亲在那里为你劬劳; 生养你的在那里为你劬劳。
6 Nitie kama muhuri moyoni mwako, kama muhuri kwenye mkono wako; kwa maana upendo una nguvu kama mauti, wivu wake ni mkatili kama kuzimu. Unachoma kama mwali wa moto, kama mwali mkubwa wa moto wa Bwana hasa. (Sheol h7585)
求你将我放在你心上如印记, 带在你臂上如戳记。 因为爱情如死之坚强, 嫉恨如阴间之残忍; 所发的电光是火焰的电光, 是耶和华的烈焰。 (Sheol h7585)
7 Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, mito haiwezi kuugharikisha. Kama mtu angelitoa mali yote ya nyumbani mwake kwa ajili ya upendo, angelidharauliwa kabisa.
爱情,众水不能息灭, 大水也不能淹没。 若有人拿家中所有的财宝要换爱情, 就全被藐视。
8 Tunaye dada mdogo, matiti yake hayajakua bado. Tutafanya nini kwa ajili ya dada yetu wakati atakapokuja kuposwa?
我们有一小妹; 她的两乳尚未长成, 人来提亲的日子, 我们当为她怎样办理?
9 Kama yeye ni ukuta, tutajenga minara ya fedha juu yake. Na kama yeye ni mlango, tutamzungushia mbao za mierezi.
她若是墙, 我们要在其上建造银塔; 她若是门, 我们要用香柏木板围护她。
10 Mimi ni ukuta, nayo matiti yangu ni kama minara. Ndivyo ambavyo nimekuwa machoni pake kama yule anayeleta utoshelevu.
我是墙; 我两乳像其上的楼。 那时,我在他眼中像得平安的人。
11 Solomoni alikuwa na shamba la mizabibu huko Baal-Hamoni; alikodisha shamba lake la mizabibu kwa wapangaji. Kila mmoja angeleta kwa ajili ya matunda yake shekeli 1,000 za fedha.
所罗门在巴力·哈们有一葡萄园; 他将这葡萄园交给看守的人, 为其中的果子必交一千舍客勒银子。
12 Lakini shamba langu la mizabibu ambalo ni langu mwenyewe ni langu kutoa; hizo shekeli 1,000 ni kwa ajili yako, ee Solomoni, na shekeli mia mbili ni kwa ajili ya wale wanaotunza matunda yake.
我自己的葡萄园在我面前。 所罗门哪,一千舍客勒归你, 二百舍客勒归看守果子的人。
13 Wewe ukaaye bustanini pamoja na marafiki mliohudhuria, hebu nisikie sauti yako!
你这住在园中的, 同伴都要听你的声音, 求你使我也得听见。
14 Njoo, mpenzi wangu, uwe kama swala au kama ayala kijana juu ya milima iliyojaa vikolezo.
我的良人哪,求你快来! 如羚羊或小鹿在香草山上。

< Wimbo wa Sulemani 8 >